Afisa Tarafa ya Katerero iliyopo Bukoba mkoani Kagera Bwanku Bwanku (katikati mwenye suti nyeusi) pamoja na Mkuu wa Polisi wa Kata ya Kemondo, Huruma Kulinganila (mwenye sare za Polisi) na maafisa watendaji kata wakiwa kwenye ziara ya kutembelea vijiwe vya bodaboda na kutoa elimu ya usalama barabarani.
................................
Na Mwandishi Wetu, Kagera
AFISA Tarafa ya Katerero iliyopo Bukoba mkoani Kagera Bwanku
Bwanku pamoja na Mkuu wa Polisi wa Kata ya Kemondo, Huruma Kulinganila na maafisa
watendaji kata wamefanya ziara ya kutembelea vijiwe vya bodaboda na kutoa elimu
ya usalama barabarani.
Akizungumza na vyombo vya habari Bwanku Bwanku alisema
wamefikia hatua hiyo ili kukabiliana ajali za pikipiki ambapo ndani ya kipindi
kisichozidi miezi miwili kata hiyo imeshuhudia ajali tatu za barabarani
zilizoua watu watatu.
“Tumeamua kutoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha
bodaboda ili kukailiana na ajali za barabarani ambazo zinatia maisha ya watu
ambao ni tegemeo kwa familia zaona taifa kwa ujumla,” alisema Bwanku.
Timu hiyo iliwahimiza waendesha bodaboda kuacha kuendesha
pikipiki zao kwa mwendo wa kasi na kuwataka kuvaa kofia ngumu maarufu kama
helmet ili ajali inapotokea ziweze kupunguza madhara kwa binadamu.
Aidha, katika ziara hiyo waliwahimiza waendesha bodaboda hao
pamoja na wananchi kuendelea kulinda amani na utulivu hasa nyakati hizi Taifa
likielekea kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu na kupuuza
wale wote wanaohubiri maandamano na machafuko.
Bwanku Bwanku akisisitiza jambo wakati wa utoaji wa elimu.
Wananchi wakisikiliza kwa makini elimu hiyo
Elimu ikitolewa







No comments:
Post a Comment