Kwa miaka mingi nilikuwa najihisi kama sauti yangu haikuwa na maana ndani ya familia yetu. Kila tulipokutana kwenye vikao vya familia, watu wengine ndio walikuwa wanaongea, wanaamua, na kutoa maoni ambayo yalichukuliwa kwa uzito.
Mimi nilikuwa kama msikilizaji tu.
Kila nilipojaribu kusema jambo, mara nyingi lilipuuzwa au kukataliwa haraka kana kwamba halikuwa na maana yoyote. Wakati mwingine nilikuwa hata nakatishwa katikati kabla sijamaliza kuzungumza. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wadogo kuniliko wakianza kuheshimiwa zaidi yangu.



0 Comments