Sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningekaa ndani ya nyumba yangu nikihisi kama nimebaki peke yangu ilhali bado nilikuwa na mume. Tulikuwa tumejenga maisha pamoja kwa miaka kadhaa. Tulikuwa tumepitia mengi changamoto za kifedha, kulea watoto, na vipindi vigumu vya maisha. Nilikuwa naamini hakuna kitu kingetikisa ndoa yetu kwa urahisi.
Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika. Mwanzoni niliona mume wangu ameanza kurudi nyumbani kuchelewa. Alikuwa anatoa sababu za kazi nyingi, meetings, au kusaidia marafiki. Nilijaribu kuelewa kwa sababu sikutaka kuwa mke wa mashaka kila wakati. Lakini kadri wiki zilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.



0 Comments