MKUU WA UPELEZI POLISI MBOZI: ACHENI TABIA ZA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI
Mkuu wa Upelelezi na Makosa ya Jinai Wilaya ya Mbozi Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Julius Kishai, akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Itewe Kata ya Itaka Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe wakati akitoa elimu juu ya madhara ya kujichukulia sheria mkononi.
.......................................
Na Issa Mwadangala (Polisi Mbozi)
WANANCHI wa Kijiji cha Itewe Kata ya Itaka Wilaya
ya Mbozi Mkoani Songwe wametakiwa kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi
pindi uhalifu unapotokea katika maeneo yao bali wametakiwa kutoa taarifa hizo
kwa Jeshi la Polisi ili ziweze kushughulikiwa kwa haraka.
Rai hiyo ilitolewa na Mkuu wa Upelelezi na Makosa
ya Jinai Wilaya ya Mbozi Mrakibu Msaidizi wa Polisi ASP Julias Kishai Aprili
23, 2024 alipofika kijijini hapo kutoa elimu juu ya madhara ya kujichukulia
sheria mkononi.
Mrakibu Kishai alisema “acheni kujichukulia
sheria mkononi toeni taarifa za uhalifu na wahalifu, katika kituo cha Polisi
kilichopo karibu nanyi ikiwa ni pamoja na kuwakamata wahalifu hao na
kuwafikisha kituo cha Polisi au kwa viongozi wa amani ili taratibu za kisheria
zichukuliwe dhidi yao.
Naye Polisi Kata wa Kata hiyo Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Kajembula Mwakalinga aliwataka wananchi wa kijiji hicho kuacha tabia ya kuziamini imani za kishilikina ambazo zinapelekea mtu kujichukulia sheria mkononi bila kufuata taratibu za kisheria ili kuepusha madhara katika jamii.
No comments