" />

HABARI ZA HIVI PUNDE

MWENYEKITI JUMUIYA YA WAZAZI TABORA : WAZAZI WAPATIENI WATOTO WENU ELIMU YA MAADILI

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wilayani Uyui mkoani Tabora Shaffin Ahmedal Suma (Aliyevaa kofia) akikabidhi vifaa mbalimbali vya kufanyia usafi kwa viongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Uyui ikiwa ni moja ya tukio la kuadhimisha siku ya jumuiya hiyo.

...........................

Na Nyamizi Moses (Singidani Blog) Tabora. 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wilayani Uyui mkoani Tabora Shaffin Ahmedal Suma amewataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanapata elimu ya kutosha na kuwalea katika maadili mema yanayopendeza katika jamii.

Shaffin Suma ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya Jumuiya ya Wazazi ya  CCM wilayani humo na kuwataka wazazi kuwa mstari wa mbele katika kufundisha vijana wao maadili mema na kupata elimu ya kutosha.     

        "Niwaombeni ndugu zangu wazazi na walezi tuhakikishe vijana wetu huko majumbani wanapata elimu inayostahili,lakini pia tuhakikishe hawa vijana wetu tunawapatia maadili mema yatakayofanya jamii ijivunie kijana wako" alisema Suma.

Suma ameongeza na kusema kuwa ni wa jibu wa Kila mzazi kusimamia makuzi bora ya mtoto wake haswa katika masomo pamoja na kuendeleza lugha adhimu ya kiswahili.    

     "Ni vyema sana kwa sisi wazazi kuwa fatilia watoto wetu hatua kwa hatua ili tuhakikishe kuwa wanafanya mambo mema katika jamii, lakini kumekuwa nwa tabia ya baadhi ya watoto wetu wanaleta tabia za nje na kuacha kuitukuza lugha yetu adhimu ya kiswahili niwaombe wazazi tu jitahidi kuwafundisha watoto utamaduni wetu pia Kuna fursa itakuja kwa watoto wetu kwenda nje kuwafundisha kiswahili lakini pasipo kujua wataendaje? kwa hiyo tulisimamie hili". alisema Suma.

Aidha ametoa zawadi kwa wa mama waliojifungua katika hospital hio ikiwa ni moja wapo ya kuunga Mkono juhudi za Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia suluhu hassan katika kuboresha huduma ya Mama na mtoto.

"jumuiya ya wazazi imeona ni vyema kutoa zawadi hizi kidogo kwa wa mama hawa waliojifungua katika hospitali hii kwahiyo kwa hiki kidogo alichotujaalia Mungu tumeona tuwape wa mama hawa" alisema Suma .

Pia Suma ametoa kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa nyumba ya mwalimu kwa shule ya  ikonola iliyopo katika kata ya isikizya wilayani Uyui.

  "Elimu ni muhimu na mimi ni muumini wa Maendeleo ya elimu katika jamii,mimi kama Mwenyekiti wa wilaya niko tayari na nitachangia Kiasi cha shilingi milioni moja ili watoto wetu wajifunze vyema na walimu waishi vyema". alisema Suma,

 Maadhimisho hayo yameambatana na upandaji miti pamoja na kutoa vifaa Vya usafi  vyenye thamani ya Sh. 400,000 katika Hospital ya Wilaya ya Uyui mkoani Tabora .

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wilayani Uyui mkoani Tabora Shaffin Ahmedal Suma, akiwasalimia wagonjwa wanaopatiwa matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Uyui.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wilayani Uyui mkoani Tabora Shaffin Ahmedal Suma akiwa amembeba mtoto wakati alipokuwa anawapa pole wagonjwa waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Wilaya ya Uyui.
Ziara katika Hospitali hiyo ikifanyika.
Ziara hiyo ikifanyika.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wilayani Uyui mkoani Tabora Shaffin Ahmedal Suma akiteta jambo na mmoja wa kiongozi wa UWT wakati wa ziara hiyo.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wilayani Uyui mkoani Tabora Shaffin Ahmedal Suma, akiwasalimia makada wa chama hicho wakati wa ziara hiyo.

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wilayani Uyui mkoani Tabora Shaffin Ahmedal Suma, akimsalimia mmoja wa wagonjwa anaye tibiwa katika hospitali hiyo.

No comments