" />

HABARI ZA HIVI PUNDE

TAASISI ZA KIISLAMU MKOA WA SINGIDA ZITAKAZO BAINIKA KUIBA WANYAMA WA SADAKA KUFUTIWA KIBALI

 Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizungumza na Waislamu wanaojishughulisha na wasimamizi wa Taasisi zinazojishughulisha na uchinjaji wa wanyama  wakati wa kusherehekea Sikukuu ya Eid ul Adha uliofanyika Mei 3, Ofisi ya Baraza Kuu la Waislamu Mkoa wa Singida.

.......................................

Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog)

SHEIKH wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro ametoa onyo kwa Taasisi za Dini ya Kiislamu zinazojishughulisha na uchinjaji wa wanyama wakati wa kusherehekea Sikukuu ya Eid ul Adha kutojihusisha na kuiba wanyama hao na itakayobaini kufanya wizi huo itachukuliwa hatua kali ikiwemo kufutiwa kibali cha kufanya kazi hiyo.

Akizungumza katika mkutano na wasimamizi wa taasisi hizo, maafisa wa Uhamiaji, wafanyabiashara wa nyama, maofisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na viongozi kadhaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Singida alisema jambo hilo la wizi wa wanyama wa sadaka halivumiliki na taasisi itakayo bainika wataishawishi Serikali kuifutia kibali taasisi hiyo.

"Suala la kuzuia uuzaji wa wanyama kiholela ni jukumu letu sote hivyo natoa onyo kwa taasisi yoyote inayojishughulisha na kazi hiyo itakayobainika wanyama wake wameuzwa tutaishawishi Serikali kukifuta kibali cha kazi hiyo dhidi ya taasisi husika," alisema Nasoro.

Aidha, Sheikh Nasoro alizitaka taasisi hizo kuchinja wanyama hao kwa kuzingatia haki ya wanyama na taratibu za dini huku wakitunza mazingira katika maeneo watakapo hifadhiwa wanyama hao kabla na baada ya kuchinjwa.

Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji Mkoa wa Singida, Diana Kisoka akizungumza kwenye mkutano huo aliwaomba wahusika wa taasisi hizo wageni wao wanaokuja kununua wanyama hao kuwaelekeza kufuata utaratibu wa nchi wa kuishi badala ya kuwapokea kiholela pasipo kuwa na vibari na baadhi yao kufikia hatua ya kuoa hadi wake wawili ili kuhalalisha ukaaji wao batili hapa nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wauza Nyama Mkoa wa Singida, Omari Palaga alisema uendeleaji wa kuchinja wanyama hao hata baada ya sherehe hiyo umekuwa ukiwaweka katika hali mbaya ya kiuchumi kufuatia kuwepo kwa nyama nyingi za bure.

"Sisi wafanya biashara wa nyama soko letu limeharibiwa na wachinjaji wa wanyama wanaoendelea kuchinja hata baada ya sherehe hiyo ya kuchinja huku tukikabiliwa na ulipaji wa kodi mbalimbali za vyumba vya biashara, TRA, usafi, gharama za kuchinja kule machinjioni na nyingine nyingi tunaomba Serikali kuliangalia jambo ili kwa undani zaidi," alisema Palaga.

Katibu wa Masheikh Mkoa wa Singida, Said Mang'ola akizungumza kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.
Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji Mkoa wa Singida, Diana Kisoka akizungumza kwenye mkutano huo kuhusu wachinjaji wanaofika kununua wanyama hao wanavyotakiwa kupata vibali vya kuwepo nchini.
Mmoja wa Masheikh akizungumza kwenye mkutano huo.
Kikao kikiendelea.
Michango mbalimbali ikitolewa kwenye mkutano huo.
Mzee Idd Mtaturu kutoka Taasisi ya JASUTA akichangia jambo kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
 

No comments