WAISLAMU SINGIDA WATEGEMEA MAGEUZI MAKUBWA KUTOKA KWA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA BAKWATA

Subscribe Us

WAISLAMU SINGIDA WATEGEMEA MAGEUZI MAKUBWA KUTOKA KWA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA BAKWATA

Mwenyekiti mpya wa Halmashauri ya BAKWATA Mkoa wa Singida, Ustadh Omary Hamisi Mughenyi

..........................................

Na Mwandishi Wetu, Singida

Mwenyekiti mpya wa Halmashauri ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Singida, Ustadh Omary Hamisi Mughenyi, ameombwa kuleta mageuzi makubwa na kuwaunganisha Waislamu ndani ya Mkoa wa Singida.

Hayo yamesemwa na Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro wakati wa hafla fupi ya kumkaribisha mwenyekiti huyo iliyofanyika Oktoba 15, 2025 mkoani hapa.

“Waislamu Singida tunahitaji ushirikiano wake, kuleta mageuzi, kutuunganisha sanjari na kushirikiana na Serikali,” alisema

Alisema matamanio ya waislamu wa Mkoa wa Singida ni kuona mabadiliko mapya ya mfumo kutoka kwenye Imani na kuelekea kwenye uchumi kwa kuwahimiza watu kufanya kazi na kujitegemea.

Katika kikao hicho, ameahidi kufanya kazi kwa karibu na viongozi wote wa mkoa na wilaya ili kuhakikisha taasisi ya BAKWATA inaendelea kuwa chombo imara cha kusimamia amani, umoja, na maendeleo ya Waislamu mkoani hapa.

Katika hafla hiyo viongozi mbalimbali waandamizi wa Bakwata mkoani hapa walihudhuria wakiwepo Katibu wa Bakwata Mkoa wa Singida, Ustadh Omary Muna, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Singida, Mzee Chief Senge na Katibu wa Baraza la Wazee, ambapo kwa pamoja walijadiliana namna bora ya kuimarisha utendaji wa taasisi hiyo.

Kikao cha ukaribisho kikifanyika
 

Post a Comment

0 Comments