Na Dotto Mwaibale, Manyoni
MKUU wa Mkoa Singida, Peter Serukamba
ameitaka kamati inayoshughulikia kilimo cha zao la korosho wilayani
Manyoni mkoani hapa kuhakikisha ifikapo Novemba 30, 2022 iwe imesafisha
mashamba na kuwapa wakulima ambao walikwisha ya yalipia lakini bado hadi leo hawajakabidhiwa.
Serukamba alitoa agizo hilo jana
wakati akizungumza na wadau wa kilimo cha zao hilo , wajumbe wa kamati ya ulinzi na
usalama na kamati inayoratibu mashamba hayo kuwa hadi ifikapo tarehe hiyo iwapo watashindwa
kufanya hivyo atawasweka ndani akiwepo
na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya
ya Manyoni.
“Hadi ifikapo Novemba 30 kama hamtakuwa mmetekeleza maagizo haya nitatumia
sheria ya kuwaweka ndani na siku hiyo nikija Takukuru, Polisi mjiandae” alisema
Serukamba.
Serukamba ameitisha kikao hicho ili
kumaliza sintofahamu ya jambo hilo linalohusisha mashamba waliopewa wakulima
hao yaliyopo Itigi-Njilii, Kaminyange, Masigati na Mkwese ambapo kuna makundi
manne ya wakulima ambao wapo kwenye mgogoro huo ulianza kutatuliwa na Serikali
mkoani hapa kwa kushirikiana na bodi ya korosho.
Makundi hayo ni la wakulima ambao walilipia mashamba hayo na wameanza
kulima, wapo wenye mashamba lakini ni mapori, wapo wenye mashamba lakini
hawajakabidhiwa rasmi na wale ambao walilipia lakini wapowapo tu na hawajui
hatima yao.
Katika kikao hicho baadhi ya wakulima walipewa nafasi ya kujieleza na kutoa masikitiko yao ya kupoteza muda mwingi wakisumbuliwa kwa zaidi ya miaka mitatu bila ya kupewa mashamba hayo licha ya kutoa fedha zao Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Melkzedeki Humbe. akizungumza kwenye kikao hicho alisema kazi kubwa inayofanyika hivi sasa ni kuyahainisha mashamba yote ambayo yalipimwa lakini hayakusafishwa na ili kuanza kumaliza mchakato huo wanatafuta fedha Sh.Milioni 450 kukamilisha kazi hiyokwa ekari zaidi ya 3120.
Mkuu wa Mkoa mstaafu wa mkoa huo Dk. Binilith Mahenge naye aliwahi kuitisha
kikao cha namna hiyo ambacho kiwahusisha Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) na kilitoa
baadhi ya maazimio kuwa ndani ya mwezi mmoja mvutano huo uwe umemalizika na
kabla ya Oktoba 1, 2022 wakulima wote waliolipia fedha zao na kukamilisha
taratibu zote wakabidhiwa mashamba yao na kuanza kulima.
Azimio lingine lilikuwa ni kutumika kwa akaunti moja ya mradi huo na kuundwa kwa kamati mpya itakayosimamia baada ya zile mbili za awali kuvunjwa na kuomba wahusika wa kamati hizo zilizovunjwa kutoa ushirikiano kwa kamati mpya na watakaoonekana wanashindwa kutoa ushirikiano watachukuliwa hatua.








No comments:
Post a Comment