SINGIDA YA 5 KWA UKATILI WA KIJINSIA KWA 31%, SHIRIKA LA CIP LAINGIA KAZINI KUPAMBANA NA HALI HIYO. - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, October 10, 2022

SINGIDA YA 5 KWA UKATILI WA KIJINSIA KWA 31%, SHIRIKA LA CIP LAINGIA KAZINI KUPAMBANA NA HALI HIYO.

Afisa Mradi wa NILINDE bw, Nice Daud  kutoka CIP akizungumza neno wakati wa kutambulisha mradi huo.
Afisa mradi wa NILINDE bw, Nice Daud  kutoka shirika Lisilo la Kiserikali la Community Initiatives Promotion  (CIP) Singida wakati wa zoezi la kutambulisha mradi.
Afisa mradi wa Nilinde GBV Project akina na Mhasibu wa Shirika wakifatilia kwa makini maelekezo ya mkurugenzi wa Singida DC..
Baadhi ya wajumbe wakifuatilia ujumbe kuhusu ukeketaji.
baadhi ya watumishi wa halamashauri ya Singida DC wakifuatilia utambulisho wa mradi.
Diwani wa kata ya Mrama.
Mhasibu wa Shirika la Community Initiatives Promotion  (CIP) Shaaban Athuman akisaini kitabu cha wageni ofisi ya mkurugenzi Singida DC.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Bi, Ester Chaula
Mwenyekiti wa Shirika la  CIP Bw, Mashanjara akizungumza wakati wa kutambulisha mradi.
Picha kati ya watumishi wa shirika la CIP na mkurugenzi wa Singida dc Ester Chaula
picha ya pamoja kati ya baadhi ya watumishi wa shirika la CIP pamoja na viongozi wa kata ya Mrama
Uzinduzi wa mradi ukiendelea.
 

Na Mwandishi Wetu, Singida 

SHIRIKA Lisilo la Kiserikali la Community Initiatives Promotion  (CIP)  lenye makao makuu yake mkoani Singida kupitia mradi wake wa Nilinde Project- lina lenga Kupunguza matukio ya ukatili wa kijinsia katika eneo la mradi ifikapo aprili 2024.

Maeneo hayo ya mradi ni Kata ya Irongelo pamoja na kata ya Mrama katika halmashauri ya wilaya ya Singida.

Akizungumza wakati wa kutambulisha mradi huo wa Nilinde afisa mradi bw, Nice Daud aliseema mradi huo utaangazia Ulinzi, Usalama na Upendo kwa wanawake na Watoto katika kata ya Ilongero na Mrama.

Alisema mradi huo ni moja ya mkakati wa uokoaji kwa wanawake na wasichana wanaoteseka na kubaguliwa kutokana na kuathirika na ukatili wa kijinsia

Bw,Nice  alisema kuwa takwimu za ripoti ya benki ya dunia juu ya tathmini ya ukatili wa kijinsia (March 2022) zinaeleza Mkoa wa Singida ulishika namba 5 (31%). Wahanga wakubwa wa UWAKI ni wanawake 15-49

Kwa mujibu ya taarifa ya ukatili wa kijinsia (Jan-December) 2021 kulikuwa na jumla ya matukio 2,511 na vitendo viovu vilivyoripotiwa mkoani Singida.

Miongoni mwa matukio hayo ni pamoja na Matukio 1,273 ya ukatili wa wanawake,Matukio 242 ya ukatili wa kihisia na,Matukio 996 ukatili wa kihisia.

Bw, Nice amesema kupitia shirika hilo la CIP  mradi huo wa Nilinde Project-Lengo kuu ni kupunguza matukio ya ukatili wa kijinsia katika eneo la mradi ifikapo aprili 2024 huku Malengo mahsusi ni pamoja na kuimarisha uelewa wa jamii katika kukabiliana na ukatili wa kijinsia,utekelezaji wa sharia na sera zinazowajibika katika kulinda na kutekeleza haki za wanawake na Watoto.

Alisema miongoni mwa mambo yanayochangia kukosekana kwa usawa wa kijinsia mkoani Singida ni pamoja kuwepo kwa mila potofu hasa, ukeketaji, utekelezaji mbovu wa sheria na sera za ukatili wa kijinsia  katika ngazi za chini,ukosefu wa uelewa kuhusu usawa wa kijinsia miongoni mwa wana jamii jambo ambalo husababisha hatua duni za usaidizi kwa wahasiriwa wa ukatili huo.

“mambo mengine ni pamoja na kuhujumu mchakato wa kisheria na kutaka kumaliza mambo ya ukatili kifamilia,ukosefu wa uelewa miongoni mwa wahanga au wahanga kuona aibu kuripoti vitendo hivyo vya ukatili wa kijinsia.”alisema Nice.

Bw,Nice aliongeza kuwa katika mradi huo wa NILINDE miongoni mwa matokeo wanayotarajia nipamoja na Kuimarisha miundombinu na taasisi zilizopo zinazoshughurikia matukio ya ukatili wa kijinsia,kuongezeka kwa idadi ya wanawake wanaomiliki rasilimali za mtaji na mali zisizohamishika katika jamii husika na Uboreshaji wa maendeleo ya taasisi.

“Mikakati mingine tuliyonayo ni Kufanya utetezi na uhamasishaji juu ya matukio ya ukatili wa kijinsia katika ngazi ya taasisi na makundi maalum,Kuhamasisha na kuimarisha uwezo wa wanawake kuhusu haki zao za kumiliki rasilimali na mali,Kushiriki katika mikutano na warsha za kujenga uwezo

Kwaupande wake mkurugenzi wa Shirika hiko la CIP Bw,Afesso Willson Ogenga amesema mbali na mradi huo wa nilinde shirika hilo limetekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na ambayo imeleta matokeo tarajiwa kwa jamii na shirika.

Bw, Ogenga alitaja baadhi ya miradi ambayo shirika hilo linatarajia kutekeleza kwa mwaka 2022-2023 kuwa ni pamoja na Kuboresha uwezo wa Watumishi wa Afya katika Utoaji Huduma,Fursa ya ufadhili wa masomo ngazi ya Diploma kwa Wauguzi na Wakunga kutoka wilaya ya Singida kozi ya mwaka 1,Mafunzo kuhusu afya ya mama na mtoto kwa wauguzi na wakunga kutoka zahanati na vituo vya Afya.

Shirika la CIP kupitia mradi wa regional cooperation kati ya mji wa Salzburg Austraria na Singida Manispaa tunaendelea kutekeleza miradi ya elimu kwa Ujenzi wa vyumba vya madarasa mashuleni,Ugawaji wa vifaa vya kujifunzia mashuleni.

Akizungumza wakati wa kutambulisha mradi huyo wa Nilinde mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Singida Bi, Ester Chaula alisema mradi huo umekuja kwa muda muafaka kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia.

“nimradi ambao umekuja wakati sahii kutokana na kuwepo kwa vitendo hivyo kwa kiasi kikubwa katika eneo letu hivyo tukishirikiana kwa pamoja tutasaidia kuongeza mapambano”

“Sisi kama serikali tutatoa ushirikiano wa kutosha ilikufanikisha lengo la mradi huo ambapo kufanikiwa kwa shirika lenu ni sawa sawa na kufanikiwa kwa serikali” 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad