HALMSHAURI YA WILAYA YA IKUNGI KUANZISHA VYANZO VIPYA VYA MAPATO BADALA YA MAZAO - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Thursday, 18 May 2023

HALMSHAURI YA WILAYA YA IKUNGI KUANZISHA VYANZO VIPYA VYA MAPATO BADALA YA MAZAO

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Ally Mwanga (katikati) akiongoza kikao cha kawaida cha baraza la madiwani cha robo ya tatu kuanzia Januari hadi Machi 2023 kilichoketi wilayani humo May 18, 2023.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Diwani wa Kata ya Mkiwa Stephen Mtyana na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Haika Masawe. 

Na Dotto Mwaibale, Ikungi

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi inatarajia kuanzisha vyanzo vipya vya mapato badala ya kutegemea chanzo cha mazao ya kilimo pekee ambacho sio cha uhakika.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Ally Mwanga wakati akifanya majumuisho katika kikao cha kawaida cha robo ya tatu kuanzia Januari hadi Machi 2023 kilichoketi May 18, 2023.

Hatua ya Mwenyekiti huyo kuzungumza hivyo ilifuatia maombi ya baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo kuwataka watalaam wa wilaya hiyo kubuni vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitaisaidia halamshauri kupata fedha za kuiendesha badala ya kutegemea ushuru wa mazao pekee na samaki.

Diwani wa kwanza kutoa ombi hilo alikuwa ni Innocent Makomelo Diwani wa Kata ya Mang’onyi ambaye alisema halmashauri hiyo haiwezi kutegemea chanzo cha mazao badala yake iangalie vyanzo vingine kama stendi za mabasi ambazo zikihimalishwa kitakuwa ni chanzo cha mapato cha kudumu.

“ Mheshimiwa Mwenyeki ifike mahala stendi yetu ya mabasi ya Ikungi ianze kufanya kazi na maeneo mengine ambayo tulipendekeza ziwepo kwani kila siku magari na watu wanasafiri tukitengeneza hizi stendi zetu na tukiweka utaratibu mzuri hizi stendi zitakuwa ni chanzo kizuri cha mapato kuliko hivi vyanzo vingine,”  alisema Makomelo.

Alisema katika kikao hicho kila diwani ambaye alikuwa akisisimama na kuulizwa mapato yaliyokusanywa anasema msimu haukuwa mzuri hivyo aliomba ombi lake la kuhimarisha vyanzo vipya vya mapato  litiliwe maanani.

Hata hivyo Makomelo alisema mjini Singida halmashauri hiyo inaeneo lao ambalo waneweza kuweka uwekezaji hata wa hoteli lakini kila wanapokutana haoni wataalam wa halmashauri hiyo wakija na mawazo na mikakati mizuri ya kueleza jinsi ya kuliendeleza na kulifanya kuwawezesha wapate fedha na kuwa mwaka huu na ujao utapita wataendelea kupewa mipango bila ya kuja na maamuzi.

“Tunawaomba waje na maamuzi tuone kama baraza hili litashindwa mheshimiwa Mwenyekiti maeneo haya ni ya kwetu hakuna mtu atakayekuja kutuamlia tunashindwa wapi’” alihoji Makomelo.

Alisema shida anayoiona hapo ni ndogo kwani mfanyabiashara anaweza kupewa Sh.Milioni 10 akafanya biashara kubwa lakini sio hao wataalam ambao wakipata bilioni moja hela hiyo itaishia kwenye mipango mikakati na michakato na mwisho kuletewa makaratasi yanayoelezea mambo mbalimbali yaliyofanyika sijui walifanya hiki na kile.

Diwani mwingine aliyechangia jambo hilo alikuwa ni Diwani wa Kata ya Iyumbu Peter Kweligwa ambaye kata yake ni maarufu kwa kilimo cha mpungu na ndio ni tegemeo kubwa la halamshauri ya Ikungi kwa kupata mapato Ikiwemo kata ya Mgungila.

Kweligwa aliomba kujengwa kwa miundombinu ya umwagiliaji kutokana na eneo lake kuwepo kwa mito mikubwa na hiyo itasaidia sana kuliko kutegemea mvua ambazo zina msimu wake.

Diwani wa Kata ya Mungaa, Gabriel Dulle aliungana na Diwani Makomelo kuhusu ujenzi wa stendi za mabasi akitolea mfano stendi ya mabasi ya Makiungu ambayo alisema inauwezo wa kuingiza zaidi ya Sh.Milioni 12 kwa mwezi lakini bado hawakioni kama ni chanzo cha mapato cha kudumu.

Diwani mwingine aliyehoji kuhusu stendi kuwa ni chanzo cha mapato cha kudumu ni Diwani wa Kata ya Ntuntu, Omari Toto ambaye alihoji fedha inayokusanywa katika stendi hiyo inachukuliwa na nani.

Wakitoa taarifa ya mapato katika kata zao baadhi ya madiwani walisema changamoto kubwa inayosababisha mapato kushuka ni kuwa na mashine chache za kukatia ushuru yaani POS na vitendea kazi vingine kama usafiri wa pikipiki na vijiji vingi kukosa watendaji wa kusimamia ukusanyaji wa mapato hayo.

Akijibu kuhusu changamoto hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Haika Masawe alisema mashine ya POS walizokuwa nazo ni 50 na sasa zimekwisha nunuliwa 10 nyingine zitakazo kwenda kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa mapato na kuwa wamepata watendaji wapya wengine 10 ambao watapangwa kimkakati kwenye vijiji ambavyo hawakuwa nao kutokana na sababu mbalimbali wakiwepo walioenda masomoni.

Masawe alisema mambo yote yaliyojiri kwenye kikao hicho yatafanyiwa kazi ili kuifanya halamshauri hiyo kuwa juu kimapato.

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Ally alisema halmashauri yoyote haiwezi kupiga hatua ya maendeleo bila ya kuwa na mapato ya kutosha hivyo madiwani wanakila sababu ya kuwa mstari wa mbele katika kukusanya mapato kwenye maeneo yao ikiwa ni pamoja na kuanzisha vyanzo vipya vya mapato.

Aidha Mwanga alisema mtendaji yeyote atakayebainika kuhujumu zoezi zima la ukusanyaji wa mapato kwa njia moja ama nyingine hawatamvumilia na kuwa atachukuliwa hatua kali.

Alisema hivi sasa ajenda yao kubwa iwe ni kukusanya mapato tena kwa nguvu zao zote ili halmashauri hiyo iwe kinara kwa kukusanya mapato mkoani hapa.

Alisema mapato ndio injini ya halmashauri hivyo ni jukumu la kila mmoja wao kuhakikisha yanakusanywa kutoka katika vyanzo mbalimbali kwani ndiyo yanayosaidia kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kutoka vyanzo vya ndani.

Katika baraza hilo madiwani walipata fursa ya kutoa taarifa mbalimbali ya matumizi ya fedha katika miradi na kujadiliana mbinu za ukusanyaji wa mapato huku kata za Mgungila, Mwaru, Ikungi na Iseke zikiwa vinara kwa ukusanyaji mapato ambapo zikipongezwa huku zile ambazo zilionekana kushuka kimapato zikitakiwa kuongeza bidii kwa kujifunza kutoka kwa zile zilizofanya vizuri.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Haika Masawe, akizungumza kwenye kikao hicho.
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Diwani wa Kata ya Mkiwa Stephen Mtyana, akichangia jambo kwenye kikao hicho. Kushoto ni  Afisa Tawala  Wilaya ya Ikungi Dijo Ndangeki
Madiwani wa Viti Maalumu, Theresia Masinjisa (kushoto) na Helena Ayubu wakipitia kabrasha wakati wa kikao hicho.
Mratibu wa Vikao wa Halmashauri hiyo Peter Bahati akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Baadhi ya watendaji wa Kata, Vijiji na Watumishi wa halmashauri ya wilaya hiyo wakiwa kwenye baraza hilo.

Baadhi ya watendaji wa Kata, Vijiji na Watumishi na wataalam mbalimbali wa wilaya hiyo wakiwa kwenye bazaza  hilo.

Baraza likiendelea.
Diwani ya Kata ya Mgungila, Deogratius Majige akitoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato katika kata yake.
Diwani wa Kaya ya Mwaru, Iddi Makangale akitoa taarifa ya mapato.
Diwani wa Viti Maalum Theresia Masinjisa akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Diwani wa Kata ya Ikungi, Abel Nkuwi akizungumza kwenye baraza hilo.
Diwani wa Kata ya Isike, Leonard Muna, akizungumza kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.

Diwani wa Kata ya Mtunduru Ramadhan Mpaki akichangia jambo kwenye baraza hilo. Kushoto ni Diwani wa Viti Maalum, Subira Kitiku.

Diwani wa Kata ya Mang;onyi, Innocent Makomelo, akizungumza kwenye kikao hicho.
Diwani wa Kata ya Iyumbu, Peter Kweligwa akizungumza kwenye kikao hicho.
Diwani wa Kata ya Ntuntu, Omari Toto akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Diwani wa Kata ya Mungaa Gabriel Dulle akichangia jambo kwenye baraza hilo.

Kikaokikiendelea.
Katibu wa Chama cha Chadema Wilaya ya Ikungi, Ibrahim Ikhalla akizungumza katika kikao hicho.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi, Stamili Dendego, akitoa salamu za chama hicho katika kikao hicho.
Diwani wa Kata ya Dung'unyi, Mathias Kasimiri akichangia jambo kwenye baraza hilo. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad