MBUNGE SINGIDA MJINI ATAKA MADIWANI WAPEWE TAARIFA ZA MIRADI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Wednesday, 10 May 2023

MBUNGE SINGIDA MJINI ATAKA MADIWANI WAPEWE TAARIFA ZA MIRADI

Mbunge wa Singida Mjini, Musa Sima, akizungumza na madiwani wa Manispaaya Singida,katika kikao baraza hilokilichofanyika mAY 10, 2023 mjini hapa. Kutoka kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo, Hassan Mkata na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Kulanga Kanyanga ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu.

Na Dotto Mwaibale, Singida

MBUNGE wa Singida Mjini, Musa Sima amehimiza madiwani wa Manispaa ya Singida wawe wanapatiwa taarifa za miradi mbalimbali inayotekelezwa katika manispaa hiyo jambo litakalo saidia kuifuatilia kwa karibu katika utekelezaji wake.

Sima ameyasema hayo katika kikao cha baraza la madiwani kilichoketi mjini hapa jana na kueleza madiwani wanapo julishwa kuhusu miradi hiyo inawasaidia kuifuatilia kwa karibu zaidi na kutekelezwa kwa ufanisi.

"Serikali chini ya uongozi wa Rais wetu Dk.Samia Suluhu Hassan inatoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo hivyo madiwani wanajukumu la kuijua ili waweze kuifutilia katika utekelezaji wake kwani ni wawakilishi wa wananchi katika maeneo inapotekelezwa miradi hiyo. 

Akizunumza katika kikao hicho Naibu Meya wa Manispaa hiyo, Hassan Mkata aliwataka madiwani kuendelea kusimamia kanuni zote wakati wa vikao vya baraza hilo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Kulanga Kanyanga ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu alisema Manispaa hiyo itaendelea kushirikiana na madiwani na wa watumishi wote ili kuipaisha  kimaendelea manispa hiyo.

Naibu Meya wa Manispaa ya Singida, Hassan Mkata akiongoza kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.
Waratibu wa Vikao wakiwa kwenye kikao hicho
Wataalamu wa Manispaa hiyo wakishiriki kikao hicho.


Kikao kikiendelea.. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Mughanga, Varelian Kimambo, Diwani wa Kata ya Uhamaka, Senge M.Senge na Diwani wa Kata ya Ipembe, Mohamed Omari Seif.
Diwani wa Kata ya Uhamaka, Senge M.Senge, akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya tatu Januari- Machi 2020/ 2023.
Diwani wa Kata ya Kisaki, Moses Ikaku akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Diwani wa Kata ya Unyianga, Geofrey Mdama, akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Diwani wa Viti Maalum Hadija Simba akiwa kwenyekikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Wataalam wa Manispaa hiyo wakishiriki kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad