Na Dotto Mwaibale, Singida
MBUNGE wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki
Kingu anatarajia kutikisa jimbo hilo mara atakapoanza ziara yake ya kikazi
baada ya bunge la bajeti kumalizika mwishoni mwa wiki.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kingu
alisema ziara hiyo haitafanana na ziara nyingine alizowahi kuzifanya kutokana na kuwa na
umuhimu mkubwa kwa wananchi wa jimbo hilo hasa baada ya kumalizika kwa bunge la
bajeti ambalo alichangia mambo mengi kwa ajili ya maslahi ya wapiga kura wake na
taifa kwa ujumla.
Akizungumzia ziara hiyo, alisema ataifanya katika
kata zote kwa kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni kutekeleza ilani ya chama
chake cha CCM na kufanya mikutano ya hadhara ambapo atasikiliza kero za
wananchi na kuzitafutia ufumbuzi na kuwa tayari ratiba ya ziara hiyo amekwisha
itoa.
"Katika jimbo la Singida Magharibi Rais
Samia Suluhu Hassan mama yetu kipenzi cha watanzania ametufanyia mambo mengi
makubwa ya maendeleo tunakila sababu ya kumshukuru na kumuombea kwa Mungu ampe
afya na maisha marefu ili aendelee kuongoza nchi yetu," alisema Kingu.
Alitaja baadhi ya miradi mikubwa iliyotekelezwa
katika jimbo hilo ni pamoja na ujenzi wa vituo vya afya cha Sepuka, Ihanja na
Igransoni, ujenzi wa barabara, shule za msingi na sekondari, umeme, maji na
minara ya simu kwa ajili ya kuimarisha mawasiliano kwa wananchi.
Kingu akitoa ratiba ya ziara hiyo alisema Julai 11, 2023 ataanza ziara hiyo Kata ya Iyumbu, na Julai 12 atakuwa Kata ya Magungumka na Julai 13 Ighombwe na Julai 25 atakuwa Kata ya Igransoni ambapo Julai 26 atakuwa Ilolo na kumalizia Kata ya Ihanja Julai 25 kwa awamu ya kwanza.









No comments:
Post a Comment