MBUNGE NGASSA: WANANCHI MSITETELEKE MPO SALAMA KWENYE MIKONO YA CHAMA CHA MAPINDUZI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, July 11, 2023

MBUNGE NGASSA: WANANCHI MSITETELEKE MPO SALAMA KWENYE MIKONO YA CHAMA CHA MAPINDUZI

Wakina mama wakimlaki Mbunge wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora, Nicholaus Ngassa wakati alipokuwa amewasilisi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jimboni humo. 

Na Mwandishi Wetu, Igunga 

MBUNGE wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora Mhe. Nicholaus Ngassa amewaomba wananchi wa jimbo hilo kutoteteleka  kwa kauli mbalimbali za upotoshaji zinazotolewa na baadhi ya watu, kuhusu maendeleo na kuwahakikishia kuwa chini ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Samoa Suluhu Hassan  wapo kwenye mikono salama na waendele kupokea miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa kupitia Ilani ya Chaka hicho.

 Ngassa ametoa kauli  hiyo wakati akizungumza na Wananchi kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara aliyofanya katika Vijiji na Vitongoji vya Kata ya Kinungu.

"Kinungu tumeleta umeme, barabara, maji ya visima  ujenzi wa miundombinu ya madarasa kwa shule zote za sekondari na msingi na sasa mjiandae kupokea maji ya Ziwa Victoria kupitia mradi unaotekelezwa kwa thamani ya Sh. Bilioni 20  kutoka kwenye tenki linalojengwa Mlima wa Bulenya.

 Watoto wanasoma elimu bure bila malipo,tumeongeza upatikanaji wa madawa na vifaa tiba kwenye vituo vya afya na zahanati za vijijini, haya ndio maendeleo tuliyoahidi mwaka 2020 kwenye kampeni na tunaendelea kutekeleza, " alisema Ngassa.

Ngassa alisema hayo yote yanatekelezwa chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye anatoa fedha nyingi nchi mzima kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

" Binafsi nichukue nafasi ya kipekee kumshukuru Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kazi hii kubwa anayoifanya kwenye jimbo letu, mkoa wetu na Taifa kwa ujumla nawaomba ndugu zangu kwa iman zetu tuendelee kumuombea kwa Mungu ampe  afya na maisha marefu," alisema Ngassa.

Katika mikutano hiyo Mbunge Ngassa alipata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali na zile zilizokuwa ndani ya uwezo wake alizitafutia ufumbuzi wa papo kwa papo kwa kushirikiana na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya  Igunga na zile zilizokuwa nje ya uwezo wake alisema ataziwasilisha kwa wahusika

Wananchi wa Jimbo la Igunga wakimshangia kipenzi Mbunge wao Nicholaus Ngassa wakati wa mikutano yake ya hadhara.
Mbunge Ngassa akipata maelezo alipotembelea moja ya Zahanati jimboni humo.
Mbunge Ngassa akisalimiana na wananchi katika moja ya mikutano jimboni humo
Mkutano ukiendelea.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad