BASI LA ALLY'S LAGONGA TRENI MANYONI NA KUUA WATU 13 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Wednesday, November 29, 2023

BASI LA ALLY'S LAGONGA TRENI MANYONI NA KUUA WATU 13

 Wananchi wakiangalia ajali iliyohusisha basi la Kampuni ya Ally's lenye namba za usajili T.178 DVB lililokuwa likitokea Jijini Dar es salaam kwenda Mwanza kugonga trni ya mizigo katika makutano ya reli na barabara kuu ya kutoka Dodoma kwenda Singida nje kidogo ya mji wa Manyoni.
Muonekano wa ajali hiyo.

...........................................................


Na Dotto Mwaibale, Manyoni

WATU 13  wamefariki dunia na wengine 32 kujeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Ally's walilokuwa wakisafiria kugonga treni ya mizigo katika makutano ya reli na barabara ya kutoka Dodoma kwenda Singida wilayani Manyoni mkoani hapa.

Ajali hiyo imetokea maji ya ya  saa 11:00 alfajiri nje kidogo na mji wa Manyoni imehusisha basi la kampuni hiyo ya Ally's yenye namba za usajili T 178 DVB lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Mwanza.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Dk.Furaha Mwakafwila, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa Hospitali ya Wilaya ya Manyoni ilipokea miili ya watu 9 waliofariki papo hapo eneo la baada ya ajali kutokea.

Alisema wengine wanne ambao ni kati ya majeruhi 32 waliopelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Manyoni na Hospitali ya St Gasper iliyopo Halmashauri ya Itigi walifariki wakati wakipatiwa matibabu katika hospitali hizo.

Mkuu wa Mkoa Singida,Peter Serukamba na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Stellah Mutahibirwa na maafisa wengine wa vyombo vya ulinzi na usalama mkoani hapa  wapo eneo la ajali.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad