POLISI KATA SONGWE: TUBADILIKE KUTOKANA NA ELIMU TUIPATAYO
Polisi Kata ya Mlangali, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Robart Kasunga, akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sembega iliyopo Kijiji na Kata ya Iyula wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe Aprili 23, 2024.
..............................
Na Issa Mwadangala, (Polisi Songwe)
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sembega iliyopo
Kijiji na Kata ya Iyula wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe wametakiwa kuzingatia
elimu wanayoipata toka kwa Walimu shuleni hapo ili kutimiza malengo ya masomo.
Rai hiyo imetolewa Aprili 23, 2024 na Polisi Kata
ya Mlangali, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Robart Kasunga baada ya kufika shuleni
hapo na kutoa elimu ya usalama kwa wanafunzi.
Mkaguzi Kasunga amewataka wanafunzi hao
kuzingatia masomo na kujiepusha na michezo ya kubahatisha (Kamali) Pool Table
na kujiepusha kutembea nyakati za usiku ili kuepuka kufanyiwa vitendo vya
ukatili.
“Tamaa ni mbaya inakatisha malengo yako hasa kwa
wanafunzi wa kike mnatakiwa kuacha tamaa za kupenda vitu vizuri ambavyo
vinapelekea mpate mimba na magonjwa na kukatisha masomo na kushindwa kufikia
ndoto za maisha yenu” alisema Mkaguzi Kasunga.
Naye, Kiongozi wa Wanafunzi wa Shule hiyo Bibianna Mitendo amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kuendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali na kuwajengea uelewa juu ya madhara ya ukatili na uhalifu na kuahidi kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili kutokomeza vitendo hivyo katika jamii.
No comments