" />

HABARI ZA HIVI PUNDE

TUNDU LISU KUUNGURUMA MKUTANO WA HADHARA SINGIDA KESHO KUTWA

Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Singida , Mutta Adrian (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu maandamano na mkutano wa hadhara utakaofanywa na chama hicho Manispaa ya Singida. Kushoto ni Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Singida, Jingu Emmanuel.

..........................

Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog)

BAADA ya vikao vya siku mbili mfululizo baina ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Singida na Jeshi la Polisi Wilaya ya Singida na Mkoa hatimaye chama hicho kimepatiwa kibari cha kuruhusiwa kufanya maandamo ya amani na kuhitimishwa kwa kufanya mkutano wa hadhara Aprili 27, 2024 Stendi ya Mabasi ya Zamani mjini hapa ambapo Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Tundu Lisu atazungumza na wananchi wa Mkoa wa Singida.

Katibu wa Chadema Wilaya ya Singida, Mutta Adrian akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandamano hayo alisema yatakuwa na msafara mmoja utakaopita barabara ya Sepuka kuanzia Uwanja wa Maonesho wa Mandewa kupitia Gineri, Uhasibu, Mataa ya FM Filling Station na maeneo mengine ya katikati ya mji kama barabara ya Arusha kupitia Serengeti, eneo la Ubungo na TCB  na kuingia kwenye Stendi hyo ya mabasi ya zamani.

Alisema maandamano hayo pamoja na  mkutano huo wa hadhara utaanza saa.2; 00 hadi saa 12;00 jioni na kuwa mkutano huo utahutubiwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Tundu Lisu atakayeambatana na viongozi wengine mbalimbali.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Singida Jingu Emmanuel alisema mkutano huo ni muhimu kwa wakazi wa Singida kwani utakuwa na ajenda tano ambazo ni kuitaka Serikali kufanya marekebisho madogo ya katiba iliyopo, kuendeleza madai ya katiba mpya ya wananchi kuitaka Serikali kushusha gharama za maisha kwa kutumia mpango wa dharura.

Emmanuel alitaja ajenda nyingine kuwa ni kuitaka Serikali kufuta au kurekebisha sheria mbovu  zilizopitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais na kuwa sheria rasmi na kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi.

Mwenyekiti huyo wa Chadema Mkoa wa Singida alitumia nafasi hiyo kuwaalika wananchi, maafiwa wa Serikali, viongozi wa dini, vyama vya siasa na makundi mengine yote kufika kwenye mkutano huo ambao utakuwa na mambo mengi ya muhimu ya kujadili mustakabari wa Taifa la Tanzania. 

Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Singida, Jingu Emmanuel akizungumzia maandamano  na mkutano huo wa hadhara.
 

No comments