" />

HABARI ZA HIVI PUNDE

DC URAMBO KUTAFUTA MUAROBAINI UHUJUMU ZAO LA PAMBA

Mkuu wa Wilaya ya Urambo ambaye pia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Elibariki Bajuta akizungumza na wananchi pamoja na Wataalamu wa Wilaya ya Urambo kuhusu zao la Tumbaku katika kikao kilichofanyika Aprili 30, 2024.

.............................

Na Nyamizi Moses, Singidani Blog, Tabora

MKUU wa Wilaya ya Urambo ambaye pia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Elibariki Bajuta amesema kumekuwa na hujuma mkubwa katika zao la tumbaku.

Kamishna Bajuta ameyasema hayo wilayani Urambo wakati akizungumza na Madiwani,Wataalamu wa  Halmashauri ya wilaya, Vyama vya Msingi, Watendaji Kata na Vijiji, Wenyeviti wa Vijiji na kusema kuwa kumekuwa na uhujumu mkubwa wa zao la tumbaku hali inayosababisha kuwepo kwa migogoro ndani ya vyama vya msingi.

Aidha, Bajuta amesema madhara yatokanayo na utoroshwaji wa Tumbaku ni Halmashauri kukosa mapato, mikopo ya banki kutorejeshwa, Vyama vya msingi kushindwa kufanya majukumu yake na wananchi kuendelea kuwa maskini.

Hata hivyo Bajuta amesema itaundwa tume maalumu ya kufatilia na kudhibiti uhujumu wa tumbaku wilayani humo.

Wananchi na Wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Taswira ya kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
 

No comments