SERIKALI YARIDHIA KUTOA FEDHA ZOTE KUMALIA UJENZI WA KITUO CHA AFYA KATA YA USAGARI
.................................
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
SERIKALI imeridhia kutoa fedha zote za kujenga Kituo cha Afya cha Kijiji
cha Migungumalo Kata ya Usagari Wilaya ya Uyui. Mkoani Tabora. Leo nina habari
nzuri kwa jimbo la Tabora Kaskazini Uyui.
Hayo yamebainishwa na Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini Uyui, Almas Maige
wakati akizungumza Bungeni jijini Dodoma mbapo pia Wizara ya
Maji nayo imeridhia maombi ya Mbunge ya kuchimba visima sehemu ambako hakuna
bomba la Ziwa Viktoria.
Maige ameyataja maeneo hayo kuwa ni Sitage Kijiji cha Mbeya Kata ya
Igulungu, Kijiji cha Katunda Kata ya Mabama, Kijiji cha Azimio Kata ya Usagari
na Kijiji cha Ndoba Kata ya Makazi.
Serikali pia Imeridhia maombi ya mbunge huyo ya kupanua Bomba la maji ya
Ziwa Viktoria kwenda vijiji vya Nsimbo, Kagera, Huyari ya Moyo na Mputi.
“ Kwa niaba ya wana Uyui Kaskazini namshukuru sana Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan kwa kuonesha upendo na kuwajali wananchi wa Uyui,” alisema Maige.
No comments