KANISA LA MORAVIAN SINGIDA LASAKA MILIONI 250 UJENZI WA MAKAO MAKUU YA JIMBO - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, May 20, 2024

KANISA LA MORAVIAN SINGIDA LASAKA MILIONI 250 UJENZI WA MAKAO MAKUU YA JIMBO

Askofu wa Kanisa la Moravian Jimbo la Magharibi Tabora, Rt Rev. Ezekiel Yona akizungumza na wakristo wa kanisa hilo Mei 19, 2024 wakati akiongoza ibada ya Pentekosti iliyofanyika na hafla ya uzinduzi wa harambee ya kupata fedha za ujenzi wa makao makuu ya kanisa hilo Jimbo la Kusini Kati Singida .

--ANGALIA VIDEO CHINI--

Na Dotto Mwaibale, Singidani Blog

KANISA la Moravian Tanzania Mission ya Singida iliyopo chini ya Jimbo la Magharibi Tabora limeanzisha harambee kwa ajili ya kupata fedha zaidi ya Sh. Milioni 250 za ujenga wa makao makuu ya jimbo hilo Kusini Kati Singida.

Akizungumza kwenye ibada ya Pentekosti iliyofanyika sanjari na uzinduzi wa harambee hiyo iliyoongozwa na Askofu wa kanaisa hilo Jimbo la Magharibi Tabora, Mchungaji Ezekiel Yona na kuhudhuriwa na Wachungaji wanafunzi zaidi ya 40 kutoka Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha kanisa hilo kilichopo Mkoa wa Mbeya kupitia umoja wao ujulikanao kama Umoja wa Wanafunzi wa Theologia (UWATHETE), Mwenyekiti wa Kamati ya ujenzi, Edward Mdaki alisema kiasi hicho cha fedha ndicho kinachohitajika ili kuanza ujenzi huo.

Alisema eneo la Mission ya Singida lilianzishwa mwaka 2017 na mpaka sasa lina miaka saba na makao makuu yake yapo Singida mjini na lina jumla ya Parishi 39, Shirika 80 na waumini wasiopungua 27,000. 

Alisema makao makuu ya jimbo hilo yatajengwa katika viwanja vya kanisa hilo eneo la Mandewa lililopo nyuma ya Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Singida.

Kiongozi wa msafara wa wanafunzi hao kutoka Chuo Kikuu cha TEKU ambaye pia ni Mhadhiri wa chuo hicho, Mchungaji Ezekiel  Majani alisema huduma ya kwenda maeneo mbalimbali ya nchi kuinjilisha waliianza miaka mitano iliyopita ambapo mwaka juzi walikuwa Mtwara, mwaka jana Rukwa na mwaka huu Mkoa wa Singida.

Mchungaji Majani alitumia nafasi hiyo kumuomba Askofu Ezekiel Yona kuwaomba viongozi wa kanisa hilo kuwasaidia kuwawezesha kupata fedha zitakazo wasaidia katika shughuli mbalimbali za uinjilishaji ikiwa ni chakula, mafuta ya gari pamoja na mahitaji mengine kwa ajili ya kufanya matendo ya huruma kwa wahitaji.

“Baba Askofu tuna changamoto kubwa ya kupata fedha za huduma hii tumekuwa tukichangishana sisi wenyewe wanafunzi jambo ambalo tunashindwa kuyafikia malengo yetu tunakuomba ukatuombee kwa viongozi wenzako,” alisema Mchungaji Majani.

Askofu Yona akipokea maombi hayo alimtaka Mchungaji Majani kuandaa mpango wa huduma hiyo ambao atauchukua na kuwapelekea viongozi wenzake ili kupata njia bora ya kuwasaidia na kuwa jambo hilo linawezekana.

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Singida ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye changizo hilo, Erick Simkwembe alisema Serikali inajua mchango mkuwa wa makanisa ambapo alitumia nafasi hiyo kuyaomba kuendelea na mchango wao wa kuyalea makundi ya vijana na wanawake katika makanisa yao.

“Baba Askofu kanisa linanafasi kubwa kuhakikisha maadili katika nchi yetu yana baki kuwa katika mstari sahihi kuna baadhi ya watu wanaweza kukemewa na kiongozi wa Serikali kuhusu ukosefu wa maadili na akawa mkali kujirekebisha lakini mtu huyo huyo akionywa na kiongozi wa dini anamsikiliza,” alisema Simkwembe.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Polisi Ushirikishi Jamii Mkoa wa Singida, ACP Hamisi Mungwana alilipongeza kanisa hilo kwa kuwa mstari wa mbele kwa mambo mbalimbali kama vile kuanzisha chuo kikuu ambacho kinatumika kutoa elimu kwa makundi ya watu mbalimbali huo ni mchango mkubwa kwa Serikali.

“Nilipongeze kanisa kwa kufanya doria ya kiroho na sisi kama jeshi la Polisi huwa tunafanya doria ya nadharia ya kutembea mitaani kuangalia usalama wa raia na mali zao nafikiri huwa munatuona,” alisema ACP Mungwana.Kiongozi wa msafara wa wanafunzi hao kutoka Chuo Kikuu cha TEKU ambaye pia ni Mhadhiri wa chuo hicho, Mchungaji Ezekiel  Majani akizungumza kwenye ibada hiyo.

Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo Mkoa wa Singida, Oscar Fallanga akiongoza ibada hiyo kama mchungaji mwenyeji.
Mkuu wa Polisi Ushirikishi Jamii Mkoa wa Sindisa, ACP Hamisi Mungwana akizungumza kwenye ibada hiyo.
Mkuu wa Polisi Ushirikishi Jamii Mkoa wa Sindisa, ACP Hamisi Mungwana akisalimiana na viongozi wa kanisa hilo baada ya kutoa mada kuhusu ushirikishwaji jamii katika masuala ya ulinzi.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Singida ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye changizo hilo, Erick Simkwembe akizungumza.
Mkuu wa Masoko Manispaa ya Singida, Philemon Kuzenza akizungumza kwenye changizo hilo.
Mwenyekiti wa UWATHETE, Mchungaji Agness Njeyo akiwatambulisha viongozi wa umoja huo.
Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi, Edward Mdaki akisoma risala kuhusu ujenzi huo. Kulia ni Katibu wa kamati hiyo, Goodluck Mashauri.
Muumini wa kwanza aliyejunga na kanisa hilo na ndugu zake 20 mkazi wa Kijiji cha Kizenge, Ibrahim Labisi akisalimiana na Askofu Ezekiel Yona. 
Mchungaji wa Kanisa la Moravian Usharika wa Singida, Yona Mbogo (kushoto) akikabidhiwa zawadi kutokana na utoaji wake wa huduma ya kiroho,. Zawadi hiyo imetolewa na UWATHETE.
Mchungaji Yona Ezekiel wa Kanisa la Moravian Parishi ya Sabasaba,(kushoto) akikabidhiwa zawadi.
Askofu Ezekieli Yona akikabidhiwa dumu la mafuta ya kula.
Mwenyekiti wa Kanisa la Moravian Jimbo la Magharibi, akikabidhiwa zawadi ya ndoo ya mafuta ya kula.
Viongozi wa kanisa hilo wakifuatilia ibada hiyo.
Viongozi wa kanisa hilo wakiwa kwenye ibada hiyo.
Viongozi wa UWATHETE wakitambulishwa.
Kwaya ya Singers ikitoa burudani.
Viongozi wa kanisa hilo wakiwa na zawadi mbalimbali zilizotolewa na UWATHETE kwa ajili ya matendo ya huruma kwa wahitajai.
Waumini wa kanisa hilo kutoka Parishi ya Sabasaba wakiwa kwenye ibada hiyo.
Watoto wa kanisa hilo wakiwa kwenye ibada hiyo.
Ibada ikiendelea.
Wanafunzi wachungaji kutoka Chuo Kikuu cha TEKU wakiwa kwenye ibada hiyo.
Wanafunzi wachungaji kutoka Chuo Kikuu cha TEKU wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Viongozi wa kanisa hilo na wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja na Baba Askofu Ezekiel Yona.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad