Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Amon Kakwale akitoa taarifa kwa waandishi wa habari.
.......................................
Na Dotto Mwaibale, Singidani Blog
JESHI Ia Polisi Mkoa wa Singida Iimeendelea
kufanya kazi zake za kulinda raia na mali zao kwa kufanya doria na misako ili
kubaini, kutanzua na kuzuia uharifu na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa 235.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna
Msaidizi Mwandamizi (SACP) Amon Kakwale akitoa taarifa kwa waandishi wa habari
alisema katika kipindi cha Februari hadi Aprili, 2024 jeshi hilo lilifanya misako
na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa 235 wa makosa mbalimbali ya jinai pamoja na
baadhi ya vielelezo vinavyo waunganisha watuhumiwa na makosa yao.
Alisema katika idadi hiyo ya watuhumiwa
walikamatwa watuhumiwa 135 wakiwa na dawa za kulevya aina ya Bhangi zenye uzito
wa Kg. 17.2, watuhumiwa 46 wakiwa na dawa za kulevya aina ya Mirungi zenye
uzito wa Kg. 92 na watuhumiwa 5 wakiwa na dawa za kulevya aina ya Heroini zenye
uzito wa gramu 0.82.
Kakwale alisema kuwa vile vile, walikamatwa
watuhumiwa 11 wakiwa na pombe ya moshi lita 123. watuhumiwa 3 wakiwa na ndoo
kubwa 31 za mafuta ya kupikia aina ya Safi mali ya Mohamed Enterprises Limited
zenye ujazo wa lita 20 kila moja. Wengine ni watuhumiwa 5 waliokamatwa na
televisheni flat screen 6, ambazo ni Hisense inchi 43 moja, Sumsung Inch 65
moja, Sumsung Inch 40 moja na tv zingine mbili zikiwa zimefutwa majina ambazo
ni mali za wizi.
CACP Kakwale alisema pamoja na hayo, walikamatwa
watuhumiwa wanaojihusisha na hujuma katika miundombinu ya umeme ambapo katika
misako hiyo walikamatwa watuhumiwa 3 wakiwa na transfoma 1 50KVA namba TX006524
aina ya TCO yenye thamani ya Tshs. 7,500,0001= na nyaya za shaba.
Pia alisema walikamatwa watuhumiwa 3 wakiwa na
miundo mbinu ya umeme wa TANESCO (polymeric post insulators) vipande 63,
ambavyo walivifunga kwenye viroba 8 tayari kwa kivisafirisha kwenda kuviuza mkoani
Mwanza na mtuhumiwa mmoja ambaye alikamatwa na mita moja ya umeme wa TANESCO.
Aliwataja watuhumiwa wengine ni pamoja na
watuhumiwa 2 ambao walikamatwa wakiwa na betri 7 za minara ya simu aina ya
NORTH STAR zenye uwezo wa N- 170 mali ya Kampuni ya HELOIS TOWER TANZANIA,
watuhumiwa 4 walikamatwa kwa kosa la kukutwa na jenereta aina ya PARKING
PORTABLE Ienye uzito wa Tani moja mali ya Kampuni ya minara ya simu ya NOVEN.
Alisema mtuhumiwa 1 kwa kosa la wizi wa matairi
matano ya gari yakiwa na rimu zake, watuhumiwa 11 kwa makosa ya wizi wa pikipiki
na watuhumiwa wanne kwa wizi wa pikipiki za magurudumu matatu (bajaji)
Alisema baada ya ukamataji huo, baadhi ya kesi
bado zipo chini ya upelelezi na zingine zimefikishwa mahakamani zikiendelea
kusikilizwa na zipo zilizopata mafanikio kwa watuhumiwa kuhukumiwa vifungo
mbalimbambali.
Kakwale alitaja baadhi ya mafanikio ya kesi
zilizofikishwa mahakamani kwa kipindi hicho ni pamoja na Mustafa Hamisi (35),
kuhukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kulawiti na kubaka. Musa
Masanilo (35), amehukumiwa kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kubaka na Baraka
Yohana (23). amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kubaka
Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida kupitia
kikosi cha usalama barabarani limefanya doria na misako na kufanikiwa
kuwakamata madereva wawili kwa makosa ya kuendesha magari kwa mwendo kasi
usioruhusiwa kisheria. Madereva hao ni Athumani Mustapha Kasenya (34), dereva
wa gari aina ya Basi lenye namba T.454 DHP mali ya Kampuni ya Matunduru na Julius Dionice (39), dereva wa gari Basi
T.937 EFK malI ya Kampuni ya SATCO.
Alisema kutokana na makosa hayo, madereva hao
walifungiwa lesenI zao za udereva kwa kipindi cha miezi mitatu kwa uendeshaji
wa gari kwa mwendo wa hatari na usiofaa jambo ambalo ni hatari kwa watumiaji
wengine wa barabara.
Kakwale kwa niaba ya jeshi hilo alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wananchi kwa kuendelea kutoa ushirikiano na kufanikisha ukamataji wa watuhumiwa hao 235 na vielelezo vilevile linawaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa zitakazosaidia kuwabaini waharifu wakamatwe mapema kabla hawajaleta madhara kwa jamii pia Jeshi la Polisi linawaomba wananchi waliopotelewa na vitu vyao vilivyotajwa hapo juu, wafike kwenye vituo vya wakiwa na risiti halisi za manunuzi ya vitu hivyo ili waweze kutambua na kukabidhiwa mali zao.








No comments:
Post a Comment