TAIFA GAS YAGAWA BURE MITUNGI 1500 KIJIJI CHA MSOMELA MKOANI TANGA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, May 18, 2024

TAIFA GAS YAGAWA BURE MITUNGI 1500 KIJIJI CHA MSOMELA MKOANI TANGA

Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga akizungumza katika hafla hiyo ya Taifa Gas kugawa bure mitungi yenge gesi kwa wananchi wa Kijiji cha Msomela Handeni mkoani Tanga.

...................................

Na Mwandishi Maalum, Msomela Tanga.

Kampuni ya Taifa Gas, imeendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ya kumtua mzigo wa kuni Mama kwa kutumia nishati safi ya kupikia na kutunza mazingira, baada ya kampuni hiyo kugawa bure mitungi 1500 yenye gesi kwa wananchi katika Kijiji cha Msomela, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Akigawa mitungi hiyo Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga alisema ameishukuru Taifa Gas na kusema  ilichofanya kampuni hiyo Msomela ni kupanda mbegu ya Mabalozi wa kudumu ambao watakuwa na wataendelea kuwa walimu wa matumizi ya Nishati safi ya kupikia na pia kuwa wateja wa kudumu wa Taifa Gas.

Naibu Waziri  amewataka Taifa Gas kuimarisha huduma hiyo ya Nishati ya gesi katika Kijiji hicho cha Msomela na maeneo jirani ili Wananchi wakiishiwa na gesi kwenye mitungi yao wasipate tabu ya mahala pa kwenda kubadilisha.

Meneja Mkuu wa Taifa Gas, Davis Deogratius alisema timu yake tayari imeshafanya mchakato wa kuwa na mawakala wazawa Msomela, hivyo gesi itakuwa ikipatikana bila wasiwasi na wale ambao hawakubahatika kupata mitungi ya Taifa Gas tayari ipo itakuwa inauzwa kwa bei nafuu.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Wakili Albart Msando aliwashukuru pia Taifa Gas kwa msaada mkubwa kwa Wananchi wake wa Msomela na aliendelea kuwaomba kuwa wananchi wake ni wengi, watapata nusu yao tu na nusu bado hivyo wakipata nafasi tena wasiwasahau Wananchi wa Msomela waliokosa.

Viongozi wakionesha furaha wakati wa ugawaji wa mitungi hiyo ya gas.
Wananchi wa Kijiji cha Msomela wakiwa kwenye hafla hiyo

Hafla ya kukabidhi mitungi hiyo ikiendelea.
Makabidhiano ya mitungi hiyo yakiendelea.
Mitungi ya gas ikikabidhiwa.
Hafla ya makabidhiano ya mitungi hiyo ikiendelea Kijiji cha Msomela.

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad