Naibu
Waziri wa Nishati Judith Kapinga akizungumza katika hafla hiyo ya Taifa Gas
kugawa bure mitungi yenge gesi kwa wananchi wa Kijiji cha Msomela Handeni mkoani Tanga....................................
Na Mwandishi Maalum, Msomela Tanga.
Kampuni ya Taifa Gas, imeendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu
Hassan, ya kumtua mzigo wa kuni Mama kwa kutumia nishati safi ya kupikia na
kutunza mazingira, baada ya kampuni hiyo kugawa bure mitungi 1500 yenye gesi
kwa wananchi katika Kijiji cha Msomela, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.
Akigawa mitungi hiyo Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga alisema
ameishukuru Taifa Gas na kusema
ilichofanya kampuni hiyo Msomela ni kupanda mbegu ya Mabalozi wa kudumu
ambao watakuwa na wataendelea kuwa walimu wa matumizi ya Nishati safi ya
kupikia na pia kuwa wateja wa kudumu wa Taifa Gas.
Naibu Waziri amewataka Taifa Gas
kuimarisha huduma hiyo ya Nishati ya gesi katika Kijiji hicho cha Msomela na
maeneo jirani ili Wananchi wakiishiwa na gesi kwenye mitungi yao wasipate tabu
ya mahala pa kwenda kubadilisha.
Meneja Mkuu wa Taifa Gas, Davis Deogratius alisema timu yake tayari
imeshafanya mchakato wa kuwa na mawakala wazawa Msomela, hivyo gesi itakuwa
ikipatikana bila wasiwasi na wale ambao hawakubahatika kupata mitungi ya Taifa
Gas tayari ipo itakuwa inauzwa kwa bei nafuu.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Wakili Albart Msando aliwashukuru pia Taifa Gas kwa msaada mkubwa kwa Wananchi wake wa Msomela na aliendelea kuwaomba kuwa wananchi wake ni wengi, watapata nusu yao tu na nusu bado hivyo wakipata nafasi tena wasiwasahau Wananchi wa Msomela waliokosa.

















No comments:
Post a Comment