WACHUNGAJI 60 KUTOKA CHUO KIKUU CHA TEKU MBEYA KUTUA SINGIDA KUFANYA UINJILISTI WA AINA YAKE - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, May 5, 2024

WACHUNGAJI 60 KUTOKA CHUO KIKUU CHA TEKU MBEYA KUTUA SINGIDA KUFANYA UINJILISTI WA AINA YAKE

Mchungaji Oscar Falanga
 

...................................

Na Mwandishi Wetu, Singidani Blog.

WACHUNGAJI Wanafunzi zaidi ya 60 kutoka Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) cha Kanisa la Moravian Tanzania kilichopo Mkoa wa Mbeya wanatarajia kufika Mjini Singida kwa ajili ya kufanya shughuli mbalimbali za uinjilisti.

Mchungaji Oscar Falanga wa Kanisa hilo Jimbo la Magharibi Tabora ambaye ni Msimamizi wa kanisa hilo Mkoa wa Singida alisema kuwasili kwa wachungaji hao mkoani Singida ni neema kubwa kwa wananchi wa mkoa huo.

Alisema mara baada ya kuwasili wachungaji hao watapata fursa ya kutoa mafunzo mafunzo ya ujasiriamali, uchumi, makuzi ya watoto haki zao na za wanawake.

Alisema ziara hiyo ya mafunzo itafanyika nyumba kwa nyumba na pia kutakuwa na matendo ya huruma ambapo watasaidia makundi yasiyojiweza na watoto yatima kwa kutoa zawadi mbalimbali.

Mchungaji Falanga alisema pamoja na mafunzo hayo wachungaji hao watafanya mikutano ya neno la Mungu kila siku katika viwanja vya Kanisa la Moraviani la Mandewa ambalo lipo nyuma ya Hospitali ya Rufaa ya Mandewa.

"Jumapilin ya Mei 19, 2024 wachungaji hao wataendesha semina na kushiriki ibada katika Kanisa Kuu la Moravian lililopo Mjini Singida.

Pamoja na mambo mengine wachungaji hao watakapokuwa mjini Singida watapata fursa ya kuonana na viongozi wa Serikali ya Mtaa na Afisa Mtendaji ambao watashirikiana nao katika masuala mbalimbali ikiwa ni  pamoja na kupata idadi ya watu kutoka makundi maalumu wakiwemo watoto yatima, wajane, wagane na wengineo kwa lengo la kuwa na idadi yao ili pindi kanisa hilo likipata nafasi liweze kuwasaidia kwa namna moja au nyingine kulingana na mahitaji watakayokuwa nayo kwa wakati husika.

Mchungaji Falanga alitumia nafasi hiyo kuwaalika wana Singida na madhehebu mengine kwenda kushirikiana na wachungaji hao kwa mambo mbalimbali kwani huduma itakayotolewa ni ya bure.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad