POLISI MANYONI WAFANYA USAFI WA MAZINGIRA KUADHIMISHA SIKU YA UTUMISHI WA UMMA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, June 22, 2024

POLISI MANYONI WAFANYA USAFI WA MAZINGIRA KUADHIMISHA SIKU YA UTUMISHI WA UMMA

Askari Polisi wa Wilaya ya Manyoni mkoani Singida wakianya usafi wa mazingira katika baadhi ya mitaa ikiwa ni kuadhimisha siku ya utumishi wa umma.

...............................

Na Mwandishi Wetu, Manyoni.

ASKARI Polisi wa Wilaya ya Manyoni mkoani Singida wamefanya usafi wa mazingira katika baadhi ya mitaa ikiwa ni kuadhimisha siku ya utumishi wa umma na kuunga mkono agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutunza mazingira.

Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Manyoni SP. Bakari Mzungu akizungumza na askari hao alisema kazi ya kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo itakuwa ni endelevu na lengo likiwa ni kuuweka mji wa Manyoni katika hali ya usafi wakati wote.

“Napenda kuwaambia na kuwakumbusha kuwa usafi ni ustarabu ambao unalinda afya zetu pamoja na mazingira tunayoishi hivyo ni wajibu wetu kujikita katika kutunza na kuyaweka katika hali ya usafi maeneo yetu yote yanayotuzunguka jambo litakalosaidia kutuepusha na magonjwa ya mlipo yanayosababishwa na uchafu,” alisema Mzungu.

Mzungu aliwataka askari hao na wana Manyoni kufanya usafi katika maeneo yao ikiwa ni kutekeleza agizo la Mkuu Wilaya hiyo Kemirembe Lwota la kufanya usafi kila Jumatano ya wiki na Jumamosi ya mwisho wa mwezi.

Mzungu alisema Polisi wanafanya usafi huo wa mazingira kwa madhumuni makubwa mawili kuadhimisha siku ya utumishi wa umma kwa kufanya kazi hiyo na wanannchi ili wawaone polisi kama watu wa kawaida jambo litakaloimarisha ushirikiano na kusaidia kuondoa uhalifu kwa kupata taarifa kutoka kwao kwa kuwa wanaofanya uhalifu huo ni watu wanaoishi nao katika jamii.

Aidha, Mzungu alitaja jambo la pili kuwa ni kuimarisha uhusiano baina yao na wananchi ambao wanawahudumia.

Usafi wa kuondoa uchafu kwenye mifereji ya kupitisha maji ukifanyika na askari hao.

Picha ya pamoja baada ya kufanya usafi katika maeneo mbalimbali wilayani humo.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad