KIWANDA CHA MSD MBIONI KUANZA KUUZA MIPIRA YA MIKONO - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, July 2, 2024

KIWANDA CHA MSD MBIONI KUANZA KUUZA MIPIRA YA MIKONO

Na Dotto Mwaibale, Njombe

KIWANDA  cha kuzalisha mipira ya mikono  cha MSD kilichopo Idofi,   Makambako mkoani Njombe  kinatarajia kuanza rasmi  kuuza bidhaa zake kwa  wadau mbalimbali hivi karibuni.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kiwanda hicho kuanza uzalishaji  Februali 12,  mwaka huu ambapo hadi  sasa tayari kimezalisha jozi milioni 2.

Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea kiwanda hicho leo kinachomilikiwa Bohari ya Dawa (MSD)  kupitia kampuni yake tanzu ya MSD Medipham Manufacturing CO LTD,  Kaimu Meneja wa kiwanda hicho, Shiwa Moshi, alisema  kina uwezo wa kuzalisha jozi (pear) 10,000.

Mbali na kampuni tanzu kumiliki kiwanda hicho,  inamiliki viwanda vingine viwili ambavyo vipo hatua za mwisho.

Viwanda  hivyo no kiwanda cha kuzalisha bidhaa za pamba kilichopo Simiyu na Zengereni cha Pwani ambacho kitakuwa kinazalisha dawa

Kwa mujibu was Moshi, kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha mipira ya mikono milioni 86.4 sawa na asilimia 83 4 ya mahitaji ya nchi.

Nae Meneja Uhusiano Mkuu was MSD, Etty Kusiluka, , alisema tayari wanelekea kuanza kuuza bidhaa zake .

Alisema kabla ya kuanzishwa kwa kiwanda hicho, MSD ilikuwa mdau mkubwa wa kununua bidhaa hizo, kuuza na kuzisamba kwa wadau, ikiwemo hosptali, vituo  na zanahati.

 Kaimu Meneja wa kiwanda hicho, Shiwa Mushi akiwaonesha waandishi uzalishaji wa mipira ya mikono (Gloves).jinsi inavyotengenezwa kwenye kiwanda hicho.
Wafanyakazi wa kiwanda hicho wakikagua mipira ya mikono(Gloves) kabla ya kuanza kusambazwa.

PICHA  ZOTE  NA  DOTTO  MWAIBALE-NJOMBE

---ANGALI VIDEO---

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad