MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA WILAYA YA MANYONI SINGIDA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Friday, 26 July 2024

MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA WILAYA YA MANYONI SINGIDA


Na Mwandishi Wetu, Manyoni 

Kila ifikapo Julai 25 ya kila Mwaka,Tanzania huadhimisha Siku ya kuwakumbuka Mashujaa waliopoteza Maisha yao wakitetea, Kuupigania na Kulinda  Uhuru wa Tanzania. Siku hii pia huambatana na Shughuli mbalimbali ikiwemo dua na sala maalumu za kuwaombea Mashujaa waliopoteza maisha  na  kuiombea Amani ya Nchi yetu Tanzania.

Mashujaa wetu walipambana kwa Hali na mali kwa ajili ya kuitetea Nchi ya Tanzania wakiwa katika Maeneo Mbalimbali, Walijizatiti na kujitoa  kwa uzalendo mkubwa kwa kuweka rehani Maisha yao kwa ajili ya Tanzania.

Uongozi na Menejimenti ya Wilaya ya Manyoni tunaungana na Watanzania wote kuwakumbuka na kuwaombea  kutokana na kujali na kudumisha Misingi ya Amani ambayo matunda yake tunayaona mpaka sasa.

Misingi mizuri na imara iliyojengwa wasisi wa Taifa letu Baba wa Taifa, Hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere Na Hayati Sheikh Abeid Amani Karume imesababisha Wananchi wa Tanzania kwa muda mrefu kuishi kwa Amani na Utulivu,huku wakifanya mambo yao kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu yeyote wa Ndani au Nje. Amani iliyojengwa na  imepelekea wageni, wakimbizi na watalii kuifanya Tanzania kuwa kivutio na kimbilio kwao.

Tuendelee kuienzi na kuilinda Amani ya Nchi yetu kwani Wapo wanaosema na kufananisha  Amani sawa na Yai mkononi ambalo ukilivunja hautaweza kulinganisha kamwe lakini pia wengine wanasema Amani  haina bei na ikipotea haina soko la kununua hivyo ni vema Tuitunze Amani yetu.

Wilaya ya Manyoni imeadhimisha siku hii kwa   kushiriki Matembezi/ Mchakamchaka kwa pamoja kufanya Usafi kuzunguka maeneo mbalimbali na Pia kuwasha mnara wa Mashujaa kama Ishara ya Kuwakumbuka na Kuwaenzi mashujaa wetu.





 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad