MAHUNDI AANZA UJENZI WA NYUMBA YA KATIBU WA UWT MKOA WA MBEYA KWA GHARAMA YA ZAIDI YA MILIONI 70 . - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, 22 September 2024

MAHUNDI AANZA UJENZI WA NYUMBA YA KATIBU WA UWT MKOA WA MBEYA KWA GHARAMA YA ZAIDI YA MILIONI 70 .

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mhe Mhandisi Maryprisca Mahundi ameanza Ujenzi wa Nyumba ya Katibu UWT Mkoa wa Mbeya kwa gharama zake zaidi ya Milioni 70 . Lengo la kujenga nyumba hiyo ni kutekeleza agizo la Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Mary Chatanda la kuzitaka kila Wilaya na Mkoa kujenga nyumba za Makatibu wa UWT pamoja na kuanzisha Vitega Uchumi.

Aidha Mhandisi Mahundi amewataka wadau wengine kujitokeza kujenga nyumba nyingine kwa UWT Kwani nafasi ipo katika kiwanja kilichopo ForestMpya Jijini Mbeya.Katika hatua nyingine amepongeza Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mbeya pamoja na viongozi wake Ndugu Edina Mwaigomole kwa kusimamia vyema mradi huo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad