Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Mayunga Mayunga akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani( pikipiki zilizokamatwa kwa makosa mbalimbali.
....................................
Imeandaliwa na Dotto Mwaibale
(0754-362990)
Jeshi la
Polisi Mkoa wa Singida katika kuimarisha ulinzi na usalama limeendelea kufanya
doria na misako ili kubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu ambapo katika kipindi
cha Mwezi Julai-August 2024 limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 137
waliojihusisha na makosa mbalimbali ya jinai pamoja na vielelezo
vinavyowaunganisha na makosa yao.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Mayunga Mayunga akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa hiyo alisema watuhumiwa hao wamekamatwa baada ya kutenda makosa tofauti tofauti.
Alitaja makosa hayo kuwa ni pamoja na mauaji watuhumiwa 21, watuhumiwa 34 kwa kukutwa na pikipiki 31 zidhaniwazo kuwa
ni za wizi, watuhumiwa 21 wakiwa na dawa za kulevya aina ya bhangi zenye uzito
wa gramu 8773, watuhumiwa 4 wamekamatwa na dawa za kulevya aina ya mirungi
zenye uzito wa gramu 19,842 na mtuhumiwa 01 akiwa na dawa za kulevya aina ya
Heroini yenye uzito wa gramu 0.5.
Alisema vilevile, walikamatwa watuhumiwa 15 wakiwa na Pombe ya Moshi lita 78, watuhumiwa 05 kwa makosa ya kubaka, watuhumiwa watatu walikamatwa kwa wizi wa kompyuta mbili, watuhumiwa watano wamekamatwa na Simu ndogo za batani 30,watuhumiwa wane wamekamatwa na mitungi miwili midogo ya gesi.
Watuhumiwa wengine ni aliyekamatwa na Tv mbili, aina ya Rising ,mtungi wa gas mdogo mmoja
, Redio subufa moja , Remote za tv tatu , m tuhumiwa mmoja amekamatwa kwa wizi
wa mifugo; mbuzi nane , watuhumiwa watatu kwa kukutwa na nyara za serikali
ambazo ni; ngozi ya mnyama aina ya Insha moja, kichwa cha mnyama aina ya Pofu mmoja, jino la mnyama aina ya Ngiri moja na
kucha moja ya mnyama aina ya Muhanga na mtuhumiwa 01 kwa kosa la kuchezesha
kamali bila kibali na mtuhumiwa mmoja akikamatwa Tv inchi 32 flat screen aina
ya zune moja.
Aidha, Kamanda
Mayunga alisema baadhi ya watuhumiwa hao wameshafikishwa mahakamani akiwemo Kamba
Kasubi ambaye ni Mganga wa Kienyeji na wenzake 13 wanaotuhumiwa kwa mauaji ya
watu watatu katika Kijiji cha Makuro Singida na mauaji ya watu saba katika
Kijiji cha Porobanguma, Wilaya ya Chemba Dodoma huku wengine upelelezi dhidi
yao ukiendelea ambapo watafikishwa mahakamani mara baada ya taratibu hizo
kukamilika.
Mayunga
alisema katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida limepata
mafanikio ya kesi zilizofikishwa mahakamani ambapo kwa mwezi Julai-August 2024
washitakiwa 43 walihukumiwa baada ya Mahakama kuridhika na ushahidi
uliowasilishwa kuhusiana na makosa ya jinai waliyoyatenda.
Hukumu hizo ni pamoja na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa washitakiwa watano wa makosa ya mauaji, washitakiwa wawili kwenda jela maisha kwa kulawiti, mshitakiwa mmoja akihukumiwa jela maisha kwa kosa la kubaka na washitakiwa wengine watano wakihukumiwa kwenda jela miaka 30 kwa makosa ya kubaka.
ACP
Mayunga alisema kwa upande wa kudhibiti makosa ya usalama barabarani, wapo
madereva waliofungiwa leseni miezi mitatu kwa makosa makubwa ya kuendesha
magari kwa mwendo kasi usioruhusiwa kisheria ambao ni hatari kwa maisha ya
abiria na watumiaji wengine wa barabara.
Madereva
hao ni Raphael Emmanue Gusha wa Kampuni ya Katarama , Habiee Neema Sule wa
Kampuni ya Mwanakwetu, Emmanuel Wilson Madaha wa Kampuni ya Katarama Luxury, Emmanuel Laizer Malambala wa Kampuni
ya Happy Nation na Jofu Mnison Kanyika wa Kampuni ya Frester ambao waliendesha
magari yao kwa mwendo wa zaidi ya Km 100 kwa saa badala ya km 80 kwa saa.
Jeshi la
Polisi Mkoa wa Singida linawashukuru wananchi kwa kuendelea kutoa ushirikiano
katika kubaini na kuzuia uhalifu na wahalifu kwa kutoa taarifa na linawaomba
kufika mahakamani kutoa ushahidi ili kesi zote ziweze kupata mafanikio.
Pia
linawataka madereva kuzingatia taratibu, kanuni na Sheria za usalama barabarani
ili kupunguza ajali ambazo zinaweza kuzuilika.







No comments:
Post a Comment