Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, ambaye alikuwa mgeni rasmi akionesha nyaraka za uzinduzi wa kampeni hiyo wakati akizungumza na wanafunzi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Kampasi ya Singida, Chuo cha Utumishi wa Umma, Chuo cha Ualimu na Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) vyote vya Singida alipokuwa akizindua Kampeni ya Tuwaambie kabla hawajaharikiwa iliyoanzishwa na Jeshi la Polisi nchini kupitia Dawati la Jinsia na Watoto.
........................
Imeandaliwa
na Dotto Mwaibale
MKUU wa Mkoa
wa Singida, Halima Dendego amewataka wakuu wa vyuo kuanzisha silabasi za malezi
kwa wanafunzi kwenye vyuo vyao ili kutoa elimu ya kuwajenga kimaadili.
Dendego
ametoa ombi hilo Oktoba 15, 2024 wakati akizungumza
na wanafunzi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Kampasi ya Singida, Chuo cha Utumishi wa Umma, Chuo cha Ualimu na
Chuo cha Maendeleo ya Wananchi.
FDC vyote vya Singida alipokuwa akizindua Kampeni ya
Tuwaambie kabla hawajaharikiwa iliyoanzishwa na Jeshi la Polisi nchini kupitia
Dawati la Jinsia na Watoto.
“Nawaombeni
anzisheni silabasi za malezi ya wanafunzi
zitasaidia kuwajenga kimaadili, zamani yalikuwepo mafunzo yaliokua yakitolewa
kwa Wasichana ambayo yalijulikiana kama unyago na kwa wavulana yalikuwa
yakiitwa jando mafunzo hayo yaliyawajenga vijana kimaadili lakini leo hii
hayapo tena,” alisema Dendego.
Alisema
uanzishwaji wa kampeni hiyo sio jambo dogo
inakwenda kukabiliana na mambo mabaya yanayotokana na utandawazi na
maendeleo yanayotokana na teknolojia.
Dendego
alisema zamani mtoto alikuwa akilelewa kuanzia ngazi ya baba, mama, mwalimu na majirani lakini leo hii mtu hawezi kumkanya
mtoto wa mtu mwingine na ndio sababu nyingine kubwa ambayo inachangia
kumomonyoka kwa maadili.
Alisema
kupitia utandawazi baadhi ya vijana wamekuwa wakikosa adamu hata kufikikia hatu
ya kumtuka Rais licha ya kufanyiwa
mipango mizuri ya maendeleo.
Mkuu huyo wa
mkoa aliwataka vijana kuacha tabia ya kujiingiza katika vitendo ambavyo
vinaweza kukwamisha ndoto zao za maisha kwa kuzingatia kuwa bado ni wategemezi
kwa kila kitu kutoka kwa wazazi wao.
“Ukitaka
kula nanasi unahitaji kuwa na nafasi na ukilila kwa pupa huwezi kulila hivyo zingatieni masomo
yenu,” alisema Dendego.
Aidha
Dendego aliwaambia wanafunzi hao kuwa miaka mitatu ya chuoni sio mingi iwapo
watafuata maelekezo ya walimu wao na kikubwa zaidi wasiache kumuomba Mungu
kupitia vipindi vya dini vinavyofanywa kila wiki katika vyuo vyao.
Aliwaambia
vijana hao kuwa wigo wa ulinzi wa maisha ya vijana hao wanaowenyewe hivyo
wasitegemee kusaidiwa na mtu mwingine.
Dendego
alisema siku hizi vifo vingi ni vya vijana na hiyo inatokana na changamoto
mbalimbali akitolea mfano ukienda mabakurini na kuangalia umri wa vijana
waliofariki wengi wao ni wale waliozaliwa kuanzia mwaka 1980, 1990 na 2000.
Mhe. Dendegu
aliwataka vijana kutumia simu zao kwa ajili ya kutangaza mambo mazuri ya
Tanzania na kueleza kuwa anapoiona Tanzania jinsi ilivyopendelewa ni kama
bustani ya Hedini ambayo ina vitu vyote kauanzia ardhi, bahari, wanyama,
madini, chakula na vingine vyote na kusisitiza kuwa watanzania hatuna nchi
nyingine mbadala wa Tanzania ambayo tunaweza kuikimbilia.
Dendegu pia
alitumia uzinduzi huo kuwataka vijana hao kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga
kura kwa ajili ya kuwachagua viongozi wanaowataka wakati wa uchaguzi wa
Serikali za Mitaa utakapo wadia ambao utafanyika hivi karibuni.
Akizungumza
kwa niaba ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa
Polisi (ACP) Mayunga Mayunga alisema mwaka 2006 jeshi la polisi lilifanya
mapinduzi makubwa ya utendaji wake wa kazi na kuwa wakisasa na uweledi na
kuanzishwa kwa polisi jamii na Dawati la Jinsia na watoto.
Mayunga
aliwaambia vijana hao kuwa wakati wote wanapsawa kuacha kujiingiza katika
vitendo vyote ambavyo vinaweza kuwaingiza kwenye changamoto mbalimbali na kuwa
mategemeo yao makubwa yawe ni kupata mafanikio.
Aliwataka
vijana hao kuacha kujiingiza katika vitendo vya ulevi, ngono zembe, matumizi ya
aina zote za dawa za kulevya, kupenda vitu vya anasa na starehe na kuwategemea
wafadhili ambao watawawezesha kupata fedha za kufanyika mambo hayo.
Kwa upande
wake Kaimu Mkurugenzi wa TIA Kampasi ya Singida, Flora Lemnge alilishukuru
jeshi la polisi kwa kuanzisha kampeni hiyo ambayo ni muhimu kwa wanafunzi hao
na kueleza kwamba inakwenda kuchochea mambano dhidi ya vitendo vyote vya
ukatili kwa wanafunzi hao.
Alisema
katika vyuo hivyo kila darasa na hosteli yupo kiongozi wa dawati wa jinsia
ambaye amekuwa akishughulikia vitendo hivyo na kuwa kila mwaka wamekuwa
wakifanya mikutano miwili ambayo wamekuwa wakikutana na wanafunzi kwa ajili ya
kuwajenga kimaadili ambayo imekuwa sanjari na michezo mbalimbali.
Mwanafunzi
wa Chuo cha Ualimu Singida, Salome Chomete na Abdi Imamu kutoka TIA Singida
wakizungumzia kampeni hiyo walisema itakwenda kuchagiza jinsi ya kumaliza kama
sio kupunguza vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia vyuoni na kuwa elimu
walioipata wanakwenda kuipeleka kwa wenzao ambao hawakubahatika kuipata.
“Wanafunzi
wengi wanapofika kuanza masomo wanakuwa na maadili mazuri na uvaaji wa nguo
wenye staha lakini wakisha kaa miezi kadhaa wanabadilika na kuanza kuvaa
nguo za ajabu hivyo naamini kupitia kampeni hii itawabadilisha,” alisema Imamu.
Uzinduzi wa
kampeni hiyo ulianza kwa maandamano yaliyohusisha wanafunzi wa vyuo mbalimba
vilivyopo mkoani Singida yalioanzia Uwanja wa Bombadia na kupokelewa na Mkuu wa
Mkoa wa Singida, Halima Dendego ukumbi wa Taasisi ya Uhasibu (TIA), Kampasi ya
Singida, ambako zilitolewa hutuba za kuwajenga wanafunzi masuala ya maadili na
burudani ya igizo, shairi na wimbo wa kizalendo kutoka Chuo cha Utumishi wa
Umma.
Maandamano ya jeshi la polisi Mkoa wa Singida na wanafunzi wa vyo hivyo yakielekea Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida kwa ajili ya uzinduzi wa kamapani hiyo.
Mlezi wa Wanafunzi wa TIA Kampasi ya Singida, Ambene Kajula akiongoza itifaki ya kukaribisha wageni wakati wa kampeni hiyo.
Heshima ya saluti ikitolewa wakati wa kuimba wimbo wa Taifa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida,Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Mayunga Mayunga akizungumza kwenye uzinduzi huo. Kaimu Mkurugenzi wa TIA Kampasi ya Singida, Flora Lemnge, akizungumza.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego akipokea maandamano hayo.
Maafisa wa Jeshi la Polisi wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Maafisa wa Jeshi la Magereza na Polisi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo.
Viongozi waandamizi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida wakiwa kwenye uzinduzi huo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Polisi Jamii, Mkoa wa Singida, ASP. Hamisi Muungwana, Mkuu wa Oparesheni Mkoa wa Singida, ACP Majura na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Singida,
Wanafunzi wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Mwanafunzi wa TIA Singida, Abdi Imamu akizungumzia uzinduzi huo.
Mwanafunzi wa Chuo cha Ualimu Singida, Salome Chomete, akizungumzia kampeni hiyo.
Askari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida wakiandamana wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo
Viongozi wakiwa meza kuu.
Taswira ya uzinduzi wa kampeni hiyo.
Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Singida wakiigiza igizo la kuzingatia maadili








No comments:
Post a Comment