SIMBA BINGWA YAGAWA KOMPYUTA 48 MAKTABA YA KIDIJITALI MUHEZA TANGA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, 1 October 2024

SIMBA BINGWA YAGAWA KOMPYUTA 48 MAKTABA YA KIDIJITALI MUHEZA TANGA

Ni katika jitihada za kuunga mkono Kauli mbiu ya "Mtoto wa leo Samia wa Kesho

Naibu Waziri Mkuu Dkt. Doto Biteko akipokea Kompyuta moja kati ya 48, zilizotolewa na Kampuni ya Simba Terminal Supply Chain Solutions ltd iliyopo chini ya Simba Bingwa kwa ajili ya Makata ya Wilaya ya Muheza katika hafla iliyofanyika wilayani humo (katikati anayeshuhudia tukio hilo) ni  Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Salha Burian.

.................................. 

Na Mashaka Kibaya Tanga.

 

KAMPUNI ya Simba Supply Chain Solutions Ltd imekabidhi Kompyuta 48 na Vifaa vya kuunganishia kwa Maktaba ya Kidijitali katika wilaya ya Muheza  ili kuhakikisha watoto wanapata nyenzo sahihi za kujifunzia, hivyo kwenda sambamba na mabadiliko ya Sayansi na teknolojia.

Hayo yamebainika Jana kwenye ziara ya Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Doto Biteko aliyoifanya wilayani Muheza Mkoani Tanga.

Taarifa hiyo imetoka Jana mbele ya Naibu Waziri Mkuu na Terminal Operation Manager wa Kampuni ya Simba Supply Chain Solution Ltd Ramadhan Hussein, alisema katika kuendeleza mkakati wa kuwa karibu na jamii Kampuni yao imetoa Komyuta 48 na Vifaa vya kuunganishia ili kuwawezesha watoto kupata nyenzo za kujifunzia hivyo kwenda sambamba na mabadiliko ya Sayansi na teknolojia .

"Katika kuendeleza mikakati yetu ya kuwa karibu na jamii leo tunashiriki hafla hii ya kuzindua Maktaba ya Kidijitali yaani Digital Library ikiwa na kauli mbiu "Mtoto wa leo Samia wa Kesho".Katika kuunga mkono kupitia Kampuni hii ya Simba Supply Chain Solutions Ltd umetoa Kompyuta 48 na Vifaa vya kuunganishia"alisema Meneja huyo wa uendeshaji.

Aidha Meneja huyo Simba Supply Chain Solutions ltd amesema kwamba,ni matumaini yake kuwa Vifaa hivyo vitatumika vyema ili kusaidia watoto hao na watu wengine kupata elimu na maarifa zaidi ili kufikia malengo yao ya maisha na hivyo kusukuma mbele maendeleo ya nchi.

Pamoja na kukabidhi msaada huo, Kampuni hiyo pia inaendesha kampeni ya utunzaji mazingira kwa kuotesha miti 23,000 katika Mkoa wa Tanga ambapo Juni 5 mwaka huu kampeni hiyo ilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Salha Burian Shule ya Msingi Pande iliyopo Wilaya ya Mkinga.

Kampuni ya Simba Terminal Supply Chain Solutions ltd ni moja ya Kampuni zilizopo chini ya Simba Bingwa Group unatoa huduma shirikishi za kibandari kwenye bandari zilizopo chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA.

Kampuni hiyo inajihusisha na umiliki,uwekezaji na uendeshaji biashara ya kutoa huduma ya kupokea mizigo,kuhudumia kwa kufungasha,utunzaji wa mizigo na usafirishaji mizigo.

Kupitia Mamlaka ya usimamizi wa Bandari, Kampuni ya Simba Terminal imekodisha eneo la Bandari ya Dar es Salaam na Tanga kwa ajili ya kuhudumia mizigo hiyo ambapo mpaka sasa Simba Terminal imefanikiwa kuleta Meli nane (8) zenye shehena mbalimbali katika Bandari ya Tanga.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad