TANESCO SINGIDA YAANZA KUADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUTEKELEZA SERA YA UZAZI SALAMA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Friday, 4 October 2024

TANESCO SINGIDA YAANZA KUADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUTEKELEZA SERA YA UZAZI SALAMA

Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Singida wakishusha maboksi yenye mashuka na mipira ya kujifungulia Wajawazito ambayo walitoa msaada ikiwa ni moja ya tukio lao kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
------------------------------------------------------

Habari Picha Dotto Mwaibale na Solomon Philemon

WAKATI Tukielekea Wiki ya Huduma kwa Wateja Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Singida limeanza kwa kutekeleza kwa vitendo sera ya uzazi salama kwa mama na mtoto.

Kaimu Meneja wa Shirika hilo Mkoa wa Singida, Mhandisi Boniface Shitindi amesema wakiwa wanaelekea wiki ya huduma kwa wateja wameamua kufika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Sindida kwa ajili ya kutoa msaada wa mashuka na mipira ya kujifungulia wajawazito.

“Moja ya Sera ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inahimiza suala zima la uzazi salama kwa mama na mtoto na sisi leo kama Shirika tumeamua kuja katika Hospitali hii kuunga mkono sera hiyo kwa kutoa mashuka na mipira ya kujifungulia wajawazito,” alisema Shitindi.

Alisema walichagua kwenda kutoa usaada huo katika hospitali hiyo ikiwa ni moja ya kutoa shukurani zao kwa wateja wao kwa kuadhimisha wiki hiyo kwa kufanya hivyo.

Aidha, Shitindi alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wateja wao kwa kuliamini shirika hilo na kulipa nafasi ya kuwahudumia kwa kuwapa ushirikiano wa kutosha ambapo pia aliwahimiza waendelee kufurahia huduma yao ya umeme kwa kutumia nishati hiyo safi kwa matumizi mbalimbali ikiwamo kujilinda kiafya na kutunza mazingira.

Kwa upande wake Katibu wa Afya wa Hospitali hiyo, Lovenes Nyange akizungumza kwa niaba ya uongozi wa hospitali hiyo alitoa shukurani za dhati kwa Tanesco Mkoa wa Singida kwa msaada huo.

Nyange alitumia nafasi hiyo kulishukuru shirika hilo kwa huduma nzuri ya nishati ya umeme wanayoitoa katika hospitali hiyo na mkoa mzima wa Singida ambapo aliyaomba mashirika, taasisi zingine za Serikali,watu binafsi na wadau mbalimbali kuiga mfano wa Tanesco kwani kuna maeneo mengi  hospitali hapo yanayohitaji msaada na kuwa Serikali peke yake haiwezi kukidhi mahitaji yote ya wagonjwa.

Wafanyakazi wa shirika hilo wakishusha mashuka hayo kutoka kwenye gari.
Kaimu Meneja wa shirika hilo, Mhandisi Boniface Shitindi, akimkabidhi mashuka hayo Katibu wa Afya wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida, Lovenes Nyange. Wengine ni wafanyakazi wa shirika hilo.
Kaimu Meneja wa shirika hilo, Mhandisi Boniface Shitindi, akimkabidhi mipira ya kujifungulia Wajawazito,Katibu wa Afya wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida, Lovenes Nyange. Wengine ni wafanyakazi wa shirika hilo.
Kaimu Meneja wa shirika hilo, Mhandisi Boniface Shitindi (kushoto), Afisa Uhusiano na Uuduma kwa Wateja (TANESCO) mkoa wa SingidaRehema Mwaipopo na Afisa wa shirika hilo Siatu wakitandika shuka katika moja ya kitanda cha wagonjwa kwenye hospitali hiyo.
Wafanyakazi wa shirika hilo wakitoka kukabidhi msaada huo.
Wafanyakazi wa shirika hilo wakionesha furaha zao baada ya kukabidhi msaada huo.
Kaimu Meneja wa shirika hilo, Mhandisi Boniface Shitindi, akizungumza wakati akikabidhi msaada huo.
Katibu wa Afya wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida, Lovenes Nyange akitoa shukurani baada ya kupokea msaada huo. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad