Mwanamuziki Maarufu Dipper Rato
Na Dotto Mwaibale
Wanamuziki wanawake wa Mkoa wa Arusha kuyapamba Maadhimisho
ya Siku ya wanawake Duniani Ambayo Kitaifa Yatafanyika Mkoa wa Arusha Kilele
cha Maadhimisho hayo ni Tarehe 8Machi 2025 Katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid
Mgeni Rasmi ni Mheshimiwa Dr Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Katibu Mkuu wa Tanzania Music Foundation (TAMUFO) Stella Joel alisema Katika
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Wanamuziki Wanawake Wa Mkoa Wa Arusha
Arusha Women Stars Wamerekodi Wimbo Maalum Uliobeba Ujumbe wa Kauli Mbiu ya
Siku ya Wanawake Duniani 2025.
Alisema wimbo huo mahususi kwenye maadhimisho hayo umelenga
kuunga mkono jitihada mbalimbali za Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia
Suluhu Hassan.
Kwa upande wake Mwanamuziki Maarufu Dipper Rato alisema wimbo
huo umeisha kamilika tna kuwa ayari wakati
wowote utaanza kusikika kwenye media mbalimbaliVyombo vya Habari.
“ Tunamshukuru Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda kwa
Kuutambua Mchango wa Wanamuziki katika Maendeleo ya Nchi Yetu na kuweza kuhamasisha
makundi mbalimbali ya Mkoa wa Arusha kushiriki shughuli za maendeleo.
Baadhi ya Wanamuziki Wanawake wa Mkoa wa Arusha wameamua kurekodi
nyimbo mbalimbali za kuhamasisha Wanachi
kudumisha Amani na Utulivu katika nchi yetu pamoja na kuhamasisha maendeleo katika
Jamii na kulinda Heshima ya Muziki na utamaduni wa Tanzania.










No comments:
Post a Comment