KWA HERI OCD AWADHI CHICO , KAPUMZIKE KWA AMANI MWEND0 UMEUMALIZA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, 18 March 2025

KWA HERI OCD AWADHI CHICO , KAPUMZIKE KWA AMANI MWEND0 UMEUMALIZA

OCD Awadhi Chico enzi za uhai wake.

....................................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

MAMIA ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake wamejitokeza kwa wingi katika mazishi ya aliyekuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi ya Chanika, Kamishna wa Operesheni ya Mafunzo Tanzania (CP) Awadhi Chico.

CP Awadhi Chico alifariki saa 1: 20 asubuhi Machi 17, 2025 katika ajali ya gari iliyohusisha daladala eneo la Pugu mwisho wa lami jijini Dar es Salaam ambalo liliacha njia na kwenda kuparamia gari dogo aina ya Prado lilokuwa likiendesha na OCD huyo na kufariki papo hapo huku mtu mwingine aliyekuwemo kwenye gari hilo akijeruhiwa.

Mazishi ya OCD Chico yamefanyika Machi 18, 2025 katika makaburi ya Kisutu huku baadhi ya waombolezaji wakimzungumzia kwa mambo mema aliyokuwa akiyafanya na kumuelezea kuwa alikuwa mtu wa watu.

OCD Chico baba yake alikuwa ni Kamanda wa Polisi katika baadhi ya mikoa hapa nchini na kuwa wakina Chico ni watoto wazawa wa Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa tayari kwa mazishi ya OCD Awadhi Chico.
Waombolezaji wakiwa kwenye shughuli hiyo ya maziko.
Viongozi mbalimbali na viongozi wa dini ya kiislamu wakiwa kwenye maziko.


Dua la kumuombea marehemu Chico ikifanyika.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad