...................................................
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Kuombea uchaguzi mkuu 2025 Ndugu Alex Msama leo Machi 15, 2025 ameongea na wandishi wa habari kuwa Maandalizi ya Tamasha la kuombea uchaguzi yanaendelea vizuri na kuwa Tamasha hilo lipo na litafanyika jijini Dar es Salaam kwa tarehe itakayotajwa na baadae kufanyika Mikoa 26 ya Tanzania.
Ameyasema hayo leo alipongea na waandishi wa Habari kuhusiana na maandalizi ya Tamasha hilo. “Maandalizi ya tamasha yanaendelea vizuri na tunakaribisha wadhamini kuja kusaidia kufanikisha Tamasha hili kubwa ambalo litafanyika Mikoa yote ya nchi yetu ya Tanzania tukianzia na Mkoa wa Dar es Salaam. Ndugu Alex Msama Mwenyekiti wa Kamati ya Mandalizi ya tamasha hilo amesema kwasasa jambo kubwa linalofanyika ni kuendelea kuzungumza na wafadhili na tukifanikiwa tu kupata wadhamini basi tamasha litakuwa halina kingilio litakuwa bule.
Tamasha la Kuombea uchaguzi litafanyika hivi karibuni na kuwaunganisha waimbaji mbali mbali wa nyimbo za injili Ndani na Nje ya Tanzania.









No comments:
Post a Comment