WANAWAKE KANISA LA MORAVIAN SINGIDA WATOA MSAADA KWA WAGONJWA HOSPITALI YA RUFAA MANDEWA SINGIDA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, March 8, 2025

WANAWAKE KANISA LA MORAVIAN SINGIDA WATOA MSAADA KWA WAGONJWA HOSPITALI YA RUFAA MANDEWA SINGIDA

Wanawake wa Kanisa la Moravian Mkoa wa Singida, wakiwa na vitu mbalimbali kabla ya kutoa kwa msaada kwa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani.

.........................................

Na Dotto Mwaibale, Singida

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Wanawake wa Kanisa la Moravian Mkoa wa Singida, wamefanya ziara maalum ya kiinjilisti ya kwenda kuwatembelea na kuwafariji wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.

Ziara hiyo iliyobeba matendo ya huruma imefanyiika ikiwa na lengo la kuwafariji, na  kuwapa misaada mbalimbali kama biblia inavyoelekeza kuwajali wenzetu waliokwenye changamoto mbalimbali zikiwemo na magonjwa.

Wanawake hao wakiongozwa na Mama Mchungaji Daniel Kikoma wamekabidhi vifaa vitu vya aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na Sukari, Sabuni, dawa za meno na vinginevyo.

Baada ya kukabidhi vitu hivyo Mama Mchungaji Daniel Kikoma aliongoza maombi  maalumu ya kuwaombea wagonjwa katika hospitali hiyo ili kupata uponyaji wa Mungu akishirikiana na Mama Mchungaji Yona Ezekiel.

Aidha baada ya kutoka hospitalini hapo walikwenda Kanisa la Moravian Sabasaba ambapo walienda ibada na kazi nyingine ikiwa ni maadhimisho ya siku yao hiyo. 

Kilele cha siku ya wanawake Duniani kitaifa kimefanyika leo Jijini Arusha, ambapo mgeni rasmi alikuwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Wanawake hao wakiwa katika picha ya pamoja.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad