MWANASHERIA CHIPAMBA: UFANISI WA SHERIA UTAKUWA WA MAFANIKIO KWA KUTOA TAARIFA ZA UHALIFU - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, 28 April 2025

MWANASHERIA CHIPAMBA: UFANISI WA SHERIA UTAKUWA WA MAFANIKIO KWA KUTOA TAARIFA ZA UHALIFU

Mwanasheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Baraka Chipamba akizungumza na wanafunzi wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Kampasi ya Temeke jijini Dar es Salaam ambavyo vipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati akifundisha kuhusu sheria mbalimbali Aprili 28, 2025.

.......................................

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

UFANISI wa Sheria mbalimbali utaendelea kupata mafanikio iwapo vitendo vya uhalifu vitakapo ripotiwa kwenye mamlaka husika na hatua kuchukuliwa.

Hayo yameelezwa Aprili 28, 2025 na Mwanasheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Baraka Chipamba wakati akizungumza na wanafunzi wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Kampasi ya Temeke jijini Dar es Salaam ambavyo vipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mwanasheria huyo aliyasema hayo wakati akitoa elimu kwa wanafunzi hao inayohusu makossa ya kimtandao ambayo yanafanywa kwa kutumia vifaa vya kieletroniki kama vile kompyuta, simu janja, vishikwambi na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)

“ Ufanisi wa sheria zetu utaendelea kupata mafanikio iwapo vitendo vya uhalifu vitaripotiwa kwenye mamlaka husika na kutolewa adhabu kwa watuhumiwa na si vinginevyo,” alisema Chipamba.

Chipamba alitaja baadhi ya makosa ya kimtandao kuwa ni kutuma picha au video za ngono kwa watoto na kuzisambaza, kuwashawishi watoto kuingilia mawasiliano ya kingono kupitia mitandao.

Alisema katika jitihada za kuimarisha ulinzi wa watoto dhidi ya makosa ya mtandao, Sheria ya Mtoto sura Na. 13, 2009  nchini Tanzania imepitia marekebisho muhimu ambayo yamezingatia athari za matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika masuala ya ulinzi wa mtoto kama vile kumlinda mtoto dhidi ya ukatili mtandaoni, kutuma lugha ya matusi, kejeli, au ya kuudhi kupitia mitandao, watoto wasidharauliwe, kusambaziwa ujumbe wa matusi au kudhalilishwa kupitia mitandao ya kijamii.

Chipamba alisema adhabu ya makossa ya kimtandao ni faini kuanzia Sh. Milioni 3 hadi Milioni 20 au kifungo cha miaka 7. Ambapo pia alihimiza mtumizi bora ya mitandao ya kijamii.

Aidha katika hatua nyingine, Chipamba alihimiza jamii kujenga tabia ya kuandika wosia kwani unasaidia kupunguza kama siyo kumaliza kabisa changamoto ya kugombea mali zilizoachwa na marehemu.

“Tujenge dhna ya kuandika wosia utatusaidia na kuondoa kabisa madhira ya kugombea mali ambazozitaachwa na marehemu,” alisema Chimpamba.

Kwa upande wake Mwanasheria Vicky Mbunde kutoka Tume hiyo, akitoa elimu kuhusu sheria ya ustawi wa wanyama alisema Serikali inawataka wananchi kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa haki za wanyama ikiwa ni pamoja na kuwapa stahiki zao.

 Alisema sheria na kanuni mbalimbali zinazolinda haki za wanyama wanaofugwa nchini zinapaswa kulindwa kwani mnyama ana haki ya kutunzwa vizuri ikiwa ni pamoja na kupewa  chakula kizuri, banda ambalo litamkinga dhidi ya mvua na jua na liwe zuri lenye mwanga wa kutosha.

“ Wanyama wana haki ya kisheria ya kutibiwa kama anavyotibiwa binadamu hivyo akiwa na changamoto yoyote ya kiafya mfugaji ana wajibu wa kumpeleka kwa daktari wa mifugo ili aweze kupatiwa matibabu na kufuata maelekezo yote yatakayotolewa na mtaalam huyo wakati wote wa matibabu yake,” alisema Mbunde.

Mbunde alisema vitendo vya kumpiga mnyama na kumnyima stahiki zake ni kosa kisheria na kuwa vinakinzana na sheria ya ulinzi na ustawi wa wanyama namba 19 ya mwaka 2008.

Meneja wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Kampasi ya Temeke, Benadeta Kessy akizungumzia elimu walioipata aliishukuru Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) kwa hatua hiyo ya kutoa mafunzo hayo kwa makundi mbalimbali ambapo aliomba elimu hiyo waipeleke kwenye kampasi zingine za LITA

Mwanasheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Vicky Mbunde akizungumza na wanafunzi wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya  Mifugo Tanzania (LITA), Kampasi ya Temeke jijini Dar es Salaam kuhusu sheria ya ulinzi na ustawi wa wanyama.
Meneja wa Wakala wa Vyuo vya  Mafunzo ya Mifugo Tanzania  (LITA), Kampasi ya Temeke, Benadeta Kessy, akiishukuru Tume hiyo kwa kuwapelekea elimu hiyo.
Mkufunzi Rajab Msami akizungumzia mafunzo hayo ambapo ameahidi kuwa watakuwa mabalozi kwa wengine.
Mwanasheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Vicky Mbunde, akitoa mafunzo kwa watumishi wa wa Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA), Kampasi ya Temeke.
Wanachuo wa kampasi hiyo wakipata elimu hiyo.
Elimu ikiendelea kutolewa.
Wanachuo hicho wakipata elimu hiyo.
Tswira ya mafunzo hayo.
Mwanafunzi Elizabeth Simon akiuliza swali.
Mwanafunzi Mussa Kilimu akiuliza swali.
Mwanafunzi Melkichezedeky Nabao akiuliza swali.
Mwanafunzi John Kichele akiuliza swali.
Wanafunzi wakipata elimu hiyo.
Wtumishi wa wakala ya Mafunzo ya Mifugo Kampasi ya Temeke, wakipatiwa elimu ya namna ya kuandika Wosia na Ufunguaji wa Mirathi.
Mafunzo kwa watumishi wa kampasi hiyo yakiendelea.
Mtumishi wa Kampasi hiyo Abdallah Mbwana akiuliza maswali mbalimbali.
Mtumishi wa Kampasi hiyo, Nuru Mhagama akitoa neni la shukurani kwa Tume hiyo kwa kuwapelekea mafunzo hayo.
Watumishi wa Kampasi hyo wakiwa katika picha ya pamoja na Wansheria kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria (LRCT), baada ya kuwapatia elimu hiyo.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad