KATIBU MKUU KIONGOZI AZIOMBA TAASISI ZA UMMA NA BINAFSI KUENDELEA KUSHIRIKIANA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Friday, 2 May 2025

KATIBU MKUU KIONGOZI AZIOMBA TAASISI ZA UMMA NA BINAFSI KUENDELEA KUSHIRIKIANA


Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, akizungumza na maafisa wa Taasisi za Umma na Binafsi kwene kikao cha mwezi kilichofanika jijini Dodoma Mei 2, 2025.

.............................................

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka ametoa wito kwa taasisis za Umma na Binafsi  kuendelea kushirikiana kwa ukaribu na kuwaamini wakaguzi wa ndani ili kusadia kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu kwa lengo la kusaidia kuondoa makosa yanayosababisha hati chafu na badala yake kuleta maendeleo chanya  katika taasisi na Taifa kwa Ujumla.

Balazi Dkt.KUSILUKA ameyasema hayo Jijini Dodoma kwenye kikao cha mwezi cha maaafisa ukaguzi wa ndani ambapo amesema ni muhimu kufanya kazi kwa kuzingatia welezdi na kufanya kazi kwa uwazi ili kufanikisha malengo ya taasisi na Taifa.

Kwa upande wake Rais wa Taasisi ya wakaguzi wa Ndani Tanzania (IIA) DKT. ZELIA NJEZA ameziomba  taasisi za Umma na Binafsi Nchini  kutoa ushirikiano kwa wakaguzi wa ndani ili wasaidie kuwapa Elimu juu uendeshaji wa  taasisi hizo ili zifanye kazi kwenye mlengo sahihi

 Kaulimbiu inayosindikiza kikao hicho cha wakaguzi wa ndani ni "Kuviwezesha Vyama. Kuimarisha Uaminifu. Kunyanyua Viwango vya Utendaji."
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, akisisitiza jambo kwene kikao hicho.
Maafisa wa Taaasisi za Umma na za Binafsi wakishiriki kikao hicho.
Picha ya pamoja.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad