Maafisa Watendaji Wakuu wa Makampuni (MA CEO) watarajiwa wakiwa katika kikao kazi kwa ajili a kujadili mikakati yao kupitia jukwaa lao la Young CEO.
...............................................
Na Mwandishi
Wetu, Singida
MAAFISA
Watendaji Wakuu wa Makampuni (MA CEO) watarajiwa wamekutanao mkoani Singida
katika kikao kazi kwa ajili a kujadili mikakati yao kupitia jukwaa lao la Young
CEO.
Mwenekiti wa
jukwaa hilo Mkoa wa Singida, Husseni Mseule akizungumza na waandishi wa habari
Manispaa a Singida Mei 9, 2025 alisema Young CEO ni platform inayo waunganisha
vijana wenye ndoto za kuwa maafisa watendaji wakuu ili kupaza sauti na kufikia ndoto
zao.
“ Young CEO ni muunganiko wa wakurungenzi vijana wanao
wasaidia vijana wenzao wenye ndoto za kuja
kuwa wakurugenzi na kufikia malengo yao na dhima ao kubwa ikiwa ni kuwaleta
pamoja kupitia fani zao mbalimbali kama ujasiriamali, wasanii, wafanya
biashara,wanamziki, Baba na Mama LISHE,saluni na wakulima huku maafisa
watendaji wakuu hao wakiwa ni waajiri wao kutokana na kuwa na uwezo wa
kuajiri,” alisema Mseule.
Mseule alisema mbeba maono na muanzilishi wa jukwaa hilo ni Jeiely
Petro (Maarufu kama Sky ) ambaye alithubutu na kuanzisha jukwaa hilo ambalo ni
la muhimu kwa vijana.
Mseule
alisema moja ya lengo la kikao hicho ilikuwa ni kubadilisha jukwaa hilo na
kuifanya kuwa taasisi ili kufungua fursa mbalimbali na wamefikia hatua hiyo
baada ya kupata ushauri kutoka kwa walezi na watu wengine ambao waliwaeleza
kuliacha jukwaa hilo au kuendelea kuwa kama kikundi ni kubana fursa na
kushindwa kupanua wigo mpana na kuwafikia vijana wengi nchini.
Alisema
maazimio ya wajumbe wa kikao hicho ni kusajili taasisi itakayojulikana kwa jina
la Global change Maker Generation (GMG) itakayosimamiwa na Singida Young CEO.
Kikao hicho
kilichofanyika KBH Hoteli kiliudhuriwa na wajumbe nane, Mwenyekiti wa jukwaa
hilo, Hussein Mseule,Katibu Moze Muna, Mweka
Hazina, Evaline Mboya, Happyness Juma, Mariam Mtaturu, Mwanzilishi wa jukwaa
hilo, Sky, Suphian Juma, Frank Musibha na walezi wa jukwaa hilo.
Kikao kikiendelea.
Wajumbe wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao hicho.











No comments:
Post a Comment