Katibu wa Mbunge, Dorice Nsekela (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Rubanga baada ya kuwakabidhi taulo kwa niaba ya Dkt. Florence Samizi Mbunge wa Jimbo la Muhambwe katika hafla iliyofanyika Juni 25, 2025.
....................................
Na Mwandishi
Wetu, Kibondo
MBUNGE wa
Jimbo la Muhambwe Dkt. Florence Samizi ametoa msaada wa taulo za kike kwa wanafunzi
wa Shule ya Sekondari ya Rubanga iliyopo Kata ya Rusohoko Wilaya ya Kibondo
mkoani Kigoma.
Baadhi ya
wanafunzi wa shule hiyo wakipokea msaada huo walisema unakwenda kuwawezesha
kuwa katika hali nzuri ya masomo na chachu ya kusoma kwa bidi na kumuahidi
mbunge huyo kuwa watafanya vizuri kwenye masomo yao na kufikia ndoto zao za
maisha.
“Tunakushukuru
sana mbunge wetu kwa msaada huu ambao umetupa mori wa kusoma pia tunaamini
utakuja tena na kutufanyia makubwa zaidi ya haya uliotufanyia,” alisema mmoja
wa wanafunzi hao.
Mkuu wa
Shule hiyo, Gervas Makunda alisema Mbunge Samizi amekuwa kiungo bora kwa
kuimarisha miundombinu ya shule hiyo hivyo kila mpenda maendeleo katika wilaya
hiyo anapaswa kumuunga mkono kwa jitihada zake hizo.
“Serikali
kupitia mbunge wetu huyu walituwezesha kutuletea maji ambayo yanatoa huduma kwa
wafanafunzi 670 huku kiasi kikubwa kikitumika kwenye vyoo na hiyo inatokana na
kujengwa eneo lenye milima,” alisema Makunda.
Alisema idadi
hiyo ya wanafunzi itaongeza na kufikia wanafunzi zaidi ya 800 hali ambayo itakuwa
ni changamoto kubwa ya maji ambapo ameiomba Serikali kupitia mbunge huyo waweze
kusaidia kuchimbiwa kisima kikubwa cha maji kwa ajili ya kukabiliana na uhaba
wa maji ya kutumia kwa kufanya usafi wa vyoo na madarasa.
“Tunamshukuru
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na mbunge wetu Dkt. Samizi kwa misaada
mbalimbali wanayoitoa kuinifaisha shule yetu kwani wangeweza kuipeleka katika
shule nyingine lakini wakaona wailete hapa kwetu Rubanga,” alisema Mwalimu
Masanja Malaba.
Wananchi wa
kata hiyo wamemuelezea mbunge huyo kuwa yupo mstari mbele kuwapambania
kuwapelekea maendeleo katika sekta mbalimbali.
“Wamepita wabunge wengi lakini hawakuwa majembe kama alivyo Florence Samizi tunapaswa kumchagua kwa kura nyingi ili aendelee kutufanyia makubwa zaidi na kama tungemchagua mwingine hizi fursa zote tunazozipata kupitia kwake tungezipata wapi?,” alihoji mmoja wa wakazi wa kata hiyo.
Wanafunzi hao wakionesha furaha zao baada ya kupokea msaada huo kutoka kwa Mpendwa Mbunge wao, Dkt. Florence Samizi..Wanafunzi wakionesha taulo baada ya kukabidhiwa.







No comments:
Post a Comment