........................................
Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
MFANYABIASHARA na Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Mbweni- Mpiji jijini Dar es Salaam, Hemed Shabani Nkunya, ambaye ametia nia ya kuwania Ubunge Jimbo la Kawe lililopo wilayani Kinondoni, leo Juni 30, 2025 amerudisha fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho ili kugombea nafasi hiyo ya ubunge.
Nkunya ambaye ni msomi wa masuala ya biashara anauzoefu katika eneo hilo pia aliwahi kuwa mjumbe wa kamati ya siasa wa CCM alipokuwa Uyui mkoani Tabora kabla ya kuhamia jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na CCM, mwisho wa kurejesha fomu kwa watia nia wote ni Julai 2, 2025.







No comments:
Post a Comment