MFANYABIASHARA HEMED NKUNYA AREJESHA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KAWE - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, June 30, 2025

MFANYABIASHARA HEMED NKUNYA AREJESHA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KAWE

Mfanyabiashara na Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya  Mbweni- Mpiji  Jijini Dar es Salaam, Hemed Shabani Nkunya (kushoto), akirejesha fomu leo Juni 30, 2025 Ofisi ya CCM Wilaya ya Kinondoni ya kuomba ridhaa ya kupitishwa na chama hicho kugombea ubunge Jimbo la Kawe.
........................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam 

 MFANYABIASHARA na Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya  Mbweni- Mpiji  jijini Dar es Salaam, Hemed Shabani Nkunya, ambaye ametia nia ya kuwania Ubunge  Jimbo la Kawe lililopo wilayani Kinondoni, leo Juni 30, 2025 amerudisha fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho ili kugombea nafasi hiyo ya ubunge.

Nkunya ambaye ni msomi wa masuala ya biashara anauzoefu katika eneo hilo pia aliwahi kuwa mjumbe wa kamati ya siasa wa CCM alipokuwa Uyui mkoani Tabora kabla ya kuhamia jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na CCM, mwisho wa kurejesha fomu kwa watia nia wote ni Julai 2, 2025.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad