Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akizungumza kwenye mkutano mkuu maalum wa CCM ambao ulifanyika jijini Dodoma kuanzia Mei 29, 2025 hadi Mei 30, 2025.
..........................................
CHAMA cha kisiasa ni maungano ya watu wanaotafuta mamlaka katika dola na hasa serikali kwa kusudi la kutekeleza shabaha za kisiasa au za kifalsafa pamoja na faida za kimaendeo kwa wanachama na wananchi.
Tanzania tangu ipate uhuru kutoka kwa wakoloni chama ambacho
kimekuwa madarakani ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) na hiyo ni kutokana na uongozi
dhabiti wa viongozi wake na sera nzuri ambazo zimekifanya chama hicho kuwa na
wanachama wengi kutokana na kujiunga nacho.
Chama
Cha Mapinduzi (CCM) ni Chama kikongwe, chenye nguvu na mvuto si kwa Tanzania tu
bali na barani Afrika na kuwa ni chama pekee cha ukombozi kilichoshiriki
kupigania uhuru katika nchi nyingi zilizokusini mwa jangwa la sahara.
Baadhi
ya nchi duniani hasa bara la Afrika zimekuwa zikifika Tanzania kujifunza namna
CCM inavyofanya shughuli zake.
Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kilianzishwa rasmi Februari 5, 1977 baada ya kuunganishwa
kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) kilichokuwa chama tawala
Tanzania Bara, kikiongozwa na Rais wa Kwanza wa Tanzania, Hayati Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere na Chama cha Afro-Shirazi Party (ASP) kilichokuwa chama
tawala Zanzibar, kikiongozwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar Sheikh Hayati Amaan
Abeid Karume.
Chama
hiki tangu kuanzishwa kwa vyama vingi mwaka 1992 kutokana na kuwa na sera nzuri
na viongozi makini kimendelea kushinda katika chaguzi mbalimbali huku kikipata
idadi kubwa ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baraza la
Wawakilishi Zanzibar.
Viongozi
walioshinda Urais kwa tiketi ya CCM kwenye chaguzi hizo ni Hayati Benjamin
Mkapa, Jakaya Mrisho Kikwete na Hayati Dk. John Joseph Pombe Magufuli na
viongozi wengine ambao wamekiongoza chama hicho kupitia nafasi ya Urais ni
Hayati Ali Hassan Mwinyi na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye aliingia
madarakani kufuatia kifo cha mtangulizi wake Hayati Dkt. John Pombe Magufuli,
Dkt.
Samia aliingia madarakani kikatiba kutokana nafasi ya makamu wa rais aliyokuwa
nayo.
Mwaka
huu Taifa la Tanzania litakuwa na tukio kubwa la uchaguzi mkuu wa kuwachagua madiwani,
wabunge na Rais ambapo vyama mbalimbali
vitashiriki uchaguzi huo baada ya kupita uchaguzi wa viongozi wa Serikali za
Mitaa,
CCM
inaingia kwenye uchaguzi huo huku ikiwa na mtaji wa wanachama zaidi ya Milioni
13 ikiwa ni ongezeko kubwa ambalo alijawahi kutokea tangu kuanzishwa kwa chama
hicho mwaka 1977.
Ongezeko
hilo la wanachama limetokana na kazi nzuri ya Mwenyekiti wa Taifa wa chama
hicho ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu
Hassan kuratibu zoezi la kitaifa la chama hicho la kusajili wanachama wote na
wapya kwa njia ya kimtandao kwa kushirikiana na watendaji wake kupitia Jumuiya
za chama hicho.
Dkt. Samia akizungumza kwenye mkutano mkuu maalum wa CCM ambao ulifanyika jijini Dodoma kuanzia Mei 29, 2025 hadi Mei 30, 2025 alisema hadi kufikia Mei 29 mwaka huu, idadi ya wanachama wa chama hicho ni 13,000,670.
Idadi hiyo kubwa ya wanachama imepatikana baada ya Dkt. Samia kuhimiza kila jumuiya kwenda kuzungumzia kazi nzuri zilizofanywa na Serikali chini ya chama hicho katika kutekeleza ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020/ 2025 ambayo imefanya mapinduzi makubwa ya maendendeleo kwenye sekta za afya, elimu, maji, barabara, umeme na maeneo mengine.
Kutokana na kunadi mafanikio hayo ya Serikali ambayo yanaonekana wananchi wakaanza kujiunga na CCM kwa makundi na kujisajili katika mfumo wa kimtandao (Kieletroniki) ulioanzishwa na Dkt. Samia ambaye alitoa vishikwambi nchi nzima kwa ajili ya kufanya kazi hiyo ambayo imezaa matunda kwa kupata wanachama hao.
Ushirikiano mkubwa wa watendaji wa chama hicho kupitia jumuiya zake na viongozi wengine ambao waliwiwa kuunga mkono jitihada za Mwenyekiti wao wa Taifa Dkt. Samia za kunadi mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya CCM na kujitoa kwao kununua simu na vishikwambi kwa ajili ya kusaidia kuongeza kasi ya kusajili wanachama zimesaidia kupatikana ongezeko hilo la wanachama.
Ziara za viongozi na mikutano ya hadhara ambayo ilikuwa ikifanyika nchi nzima kuanzia viongozi wa juu wa kitaifa wa CCM, kusiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi, kukagua miradi ya maendeleo na kuelezea mafanikio ya Serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo zimesaidia kuwafanya wananchi na wanachama wa vyama vingine kuiamini Serikali na kujiunga na chama hicho.
WANA CCM WANAZUNGUMZIAJE ONGEZEKO HILO LA WANACHAMA
Makamu Mwenyekiti wa Chama
cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Stephen Wasira, alisema idadi kubwa ya
wanachama waliosajiliwa ndani ya chama hicho inatosha kukifanya CCM kuendelea
kushika dola na kubaki madarakani.
Wasira alitoa kauli hiyo
Januari 23, 2025, baada ya kupokewa na wanachama wa CCM Makao Makuu ya chama
hicho, jijini Dodoma.
Akizungumza mbele ya mamia ya
wanachama waliojitokeza, Wasira alisema, "Kwa mtaji wa wanachama
tuliowasajili, CCM ina nguvu ya kuendelea kushika madaraka na kuleta maendeleo
endelevu kwa Watanzania."
Akiwa kwenye mkutano huo,
Wasira aliwakumbusha wanachama na viongozi kuwa mwaka 2025 ni mwaka muhimu wa
uchaguzi wa Rais, Wabunge, na Madiwani, na hivyo aliwataka wanachama waendelee
kuwa imara na kushirikiana kuhakikisha chama kinapata ushindi wa kishindo.
"Huu ni mwaka wa uchaguzi, ni lazima tuhakikishe tunadumisha mshikamano, tukitekeleza sera zetu kwa ufanisi, na kuendelea kuwahudumia Watanzania kwa uadilifu," alisema Wasira.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Michael Lushinge Masanja (Smart), ambaye naye kwa namna moja alichangia vishikwambi kwa ajili ya kusaidia kusajili wanachama alipokuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Misungwi alianza kwa kumshuru Mwenyekiti wa Taifa wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha jambo hilo baada ya kulichukulia uzito mkubwa kwa kuliwezesha na wao kama chama wanajivunia sana jambo hilo la msingi.
“Sisi wafanyabiashara mtaji
wetu ni kuwa na rasilimali ya wateja kwani ili kujua kama imekuwa ni ile idadi ya watu
inayoongezeka na halikadharika mtaji
mkubwa wa siasa ni kuwa na wanachama wengi na hasa wakati huu tunapoingia kwenye
uchaguzi mkuu tunajivunia kuwa na wingi wa wanachama,” alisema Smart .
Alisema kwanza tu wana mtaji
wa wanachama zaidi ya Milioni 13 hapo bado marafiki, ndugu, jamaa wa wanachama
hao huku akijitolea mfano kuwa katika shughuli zake za biashara ameajiri watu
karibu 300 ambao wanamuombea mema huku akisisitiza kuwa wafanyakazi wake hao na
wao wana marafiki zao ambao moja kwa moja watakuwa ni sehemu ya wanachama hao hivyo
wanajivunia sana.
“Tunampongeza Mhe. Rais
mafanikio yake ni makubwa sana kwa haraka haraka chama chetu kinakwenda kuwa na
rasilimali ya wanachama zaidi ya Milioni 20 hapo hakuna muujiza wa kumfanya mtu
ajitokeze akilalamikia ushindi wa CCM kwani mtaji tulionao ni mkubwa mno,”
alisema.
Katibu wa CCM Wilaya ya
Nkinga, Stamili Dendego alisema kazi kubwa aliyoifanya mwenyekiti wao Taifa ni
kubwa mno hasa katika ongezeko la wanachama ambao ni mtaji mkubwa katika uchaguzi
mkuu.
“Idadi hiyo itaendelea
kuongezeka kutokana na maelekezo tuliyopewa katika mkutano maalum uliofanyika
jijini Dodoma,” alisema Dendego.
Mwana CCM na Mdau wa Maendeleo, Joseph Nyarandu
kutoka Kintiku Wilaya ya Manyoni Mkoa wa Singida, alisema wanajivunia uimara
wa CCM na Serikali chini ya Rais Samia kwa uongozi dhabiti na wa wazi ndio
unaokifanya chama hicho kupendwa na
kukimbiliwa na watu wengi.
“CCM kimejengwa kwa misingi
ya demokrasia, utu na kujali maslahi ya watu wote pasipo ubaguzi wa aina yoyote ni chama chenye viongozi
wenye weledi wa hali ya juu na ni chama cha mfano,” alisema Nyarandu.
Alisema ongezeko hilo la
wanachama ni kazi nzuri anayoifanya Rais Samia ya kukijenga na kukiimarisha
chama hicho na kukifanya kuwa cha kisasa zaidi hivyo wanajivunia mafanikio
hayo.
Kwa upande wake Katibu wa CCM
Wilaya ya Chamwino, Ibrahim Said Mpwapwa alimshukuru Mwenyekiti wa chama
hicho Taifa Dkt. Samia kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kukiwezesha vitendea kazi
hasa usafiri wa magari, pikipiki na baiskeli jambo ambalo limewafanya watendaji
wa chama hicho kupitia jumuiya zake kufika kila sehemu kutekeleza majukumu yao.
“ Jambo hili la kuwezeshwa vifaa
vya usafiri limechagiza kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi hiyo ya wanachama
hakika tunamshukuru sana mwenyekiti wetu,” alisema Mpwapwa.
Alisema jambo lingine ambalo
limewafanya wananchi kukiamini chama hicho na kujiunga nacho ni Serikali chini
ya CCM jinsi ilivyofanya kazi kubwa ya kutekeleza miradi mbalimbali ya
maendeleo huku mingine ikiwa imekwisha kamilika.
Naye Katibu wa CCM
Wilaya ya Ruangwa, Abbas Mkweta alisema ili chama kiwe hai ni lazima kiwe na
wanachama hivyo kupata idadi hiyo ya wanachama kinaonesha jinsi chama kilivyo
na nguvu na hai..
“Jambo hili haliji tu hivi
hivi bali inatokana na kazi nzuri iliyofanyika kama unavyojua hivi sasa siasa
ni kama biashara ambayo inakuwa na ushindani kwani ukipeleka bidhaa mbovu
sokoni hakuna mteja ambaye ataweza kununua na ndivyo ilivyo hata kwenye siasa
sisi bidhaa zetu ni huduma,” alisema Mkweta.
Alisema kama chama wanatoa
huduma kwa wananchi kama walivyoahidi na yamefanyika kwa kiwango kikubwa hivyo
watanzania wengi kuvutiwa na chama hicho na hilo ndio jambo kubwa.
Alisema Rais Samia alipokuwa
anaachiwa nchi kutoka kwa mtangulizi wake Hayati Dkt. John Pombe Magufuli
kufuatia kifo chake kuna watu walimbeza kuwa ni mwanamke hataweza lakini
tumeona jinsi anavyoiongoza nchi kwa misimamo yake na uimara na hatua ambazo
amekuwa akizichukua pale anapoona mambo hayaendi sawa.
Alisema wakati anaingia
madarakani baadhi ya watu walikuwa na mashaka naye lakini chini ya uongozi wake
nchi imetulia, kuna usalama wa kutosha na amefanikiwa kutekeleza miradi
mbalimbali ya maendeleo kwa kiwango cha juu na mingine ikiendelea.
Alitaja baadhi ya miradi hiyo ni Bwawa la kufua umeme la Nyerere, Daraja la Kigongo la Busisi, Reli ya Kisasa ya SGR, Daraja la Selander hiyo na kuwa hiyo ni sehemu ya miradi ya Dar es Salaam na kwa Wilaya ya Ruangwa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Nanganga hadi Ruangwa mjini jambo ambalo linawafanya wananchi wafurahi na kusafirisha mazao yao ya biashara kama korosho, ufuta, mbaazi na mengineyo ya chakula.
Mwana CCM na Mdau wa maendeleo wa chama hicho kutoka Mkoa wa Mara Mhandisi Yazid Mabala alisema ongezeko hilo la wanachama ni mtaji mkubwa wa CCM huku akielezea kwamba katika sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 watanzania wote walikuwa ni Milioni 61, 841, 924 watoto chini ya miaka 18 wakiwa ni Milioni 30, 257, 196 na watu wenye umri wa kupiga kura ambao walikuwa na umri kuanzia miaka 18 kwenda juu wakiwa ni Milioni 31, 583, 924.
Alisema kwa takwimu hizo inaonesha wana CCM ambao wapo juu ya umri wa kupiga kura ni asilimia 41. 2 hivyo tafsiri yake kisiasa chama hicho kitaingia kwenye uchaguzi tayari kikiwa na wanachama ambao watakuwa ndani ya chama hicho.
“ Hii ni hazina kubwa ya chama chetu kutokana na watu
kukielewa kwa kila kitu kwani iwapo kutakuwa na wapiga kura 100 CCM tutakuwa na
asilimia 41 ya wapiga kura ambao hawatingishiki, hawahami na wapo na chama
hicho kihisia na kiitikadi,” alisema Mabala.
Aliongeza kuwa asilimia ya wanachama hao waliobaki watafanya
mikakati mbalimbali ili kuongeza asilimia hizo zilizobaki na kukifanya chama
hicho kupata ushindi.
Alisema CCM ilijenga imani kubwa kupitia kusajili wanachama na kukifanya
kieleweke na ongezeko hilo ni faida kubwa kwa chama hicho hasa kwa Dkt. Samia
ambaye alikuja na mkakati huo wa kusajili wanachama ambao umekiimarisha.
Alisema mkakati wa kwanza aliokuja nao Dkt. Samia ni kununua
simu nne ambazo zilipekekwa katika kila kata nchi nzima huku kila eneo likiwa
na mkakati wake na kauli mbiu za kuhamasisha watu kujisajili ambapo kwa Mkoa wa
Mara walikuwa na kauli mbiu yao waliyoipa jina la siku kumi za moto za mama iliyokuwa
na lengo la kutoa hamasa watu kwenda kujisajili na kuwekwa kwenye kanzidata kwa
ajili ya kutambulika.
Makala hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu (O754362990)
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa kwenye mkutano huo.
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakishiriki katika mkutano huo.

.jpeg)
.jpeg)








No comments:
Post a Comment