HAIDERALI GULAMALI: UMOJA NDIYO UNAIFANYA CCM KUENDELEA KUSHIKA DOLA

Subscribe Us

HAIDERALI GULAMALI: UMOJA NDIYO UNAIFANYA CCM KUENDELEA KUSHIKA DOLA

Mgombea Nafasi ya Ubunge , Haiderali Gulamali wa  Jimbo la Ilongero lililopo Wilaya ya Singida mkoani Singida akihutubia wananchi na Wana CCM wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu 2025 jimboni humo.

.................................................

 Dotto Mwaibale na Philemoni Solomon Singida

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinaendelea kushika dola kwa sababu ya umoja uliojengeka tangu nchi yetu ipate uhuru.

Hayo yamesemwa na Mgombea Nafasi ya Ubunge, Haiderali Gulamali wa  Jimbo la Ilongero lililopo Wilaya ya Singida mkoani Singida wakati akihutubia wananchi na Wana CCM wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu 2025.

“ Tuliojitokeza kugombea nafasi ya ubunge tulikuwa wengi lakini mnaona jinsi wenzangu ambao hawakubahatika kuchaguliwa walivyofika kuniunga mkono na wengine wamevuka mpaka kwa kutoa fedha zao kuwachangia madiwani,” alisema Gulamali.

 Gulamali aliongeza kuwa hicho ndiyo Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho kila Mwana Ilongero na watanzania wanajivunia uwepo wake.

Gulamali alisema kuwa chama hicho kinaendelea kushika dola kutokana na demokrasia na uwazi ilionao ndani ya chama hicho kikubwa si kwa Tanzania pekee bali na Afrika kwa ujumla.

Alisema amegombea nafasi hiyo siyo kwa ajili ya kupata fedha bali kuwiwa kuwatumikia wana Ilongero na wananchi kwa ujumla.

Alitumia nafasi hiyo kukishukuru chama hicho kwa kumuamini kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa ambapo ameahidi kuwatumikia wananchi kadri atakavyo jaaliwa na Mwenyezi Mungu.

Gulamali atakuwa  mbunge wa kwanza wa jimbo hilo jipya la Ilongero zamani likiitwa Jimbo la Singida Kaskazini.

Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri mstaafu Wizara ya Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akizungumza kwenye uzinduzi huo aliwataka kila mwananchi mwenye kadi ya kupigia kura kujitokeza kwenda kupiga kura nyingi kwa wagombea wanaotokana na CCM kuanzia za Rais, wabunge na madiwani.

“Tunahitaji Mkoa wa Singida uwe kinara wa kura zote katika uchaguzi mkuu na hilo linawezekana kutokana na umoja wetu tulionao”, alisema Nyalandu huku akishangiliwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata alisema demokrasia iliyomo ndani ya chama hicho ndiyo inakifanya kionekane tofauti na vyama vingine kutokana na kuwapata viongozi wake kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa kwa kuchaguliwa.

Mgombea Nafasi ya Ubunge, Haiderali Gulamali wa  Jimbo la Ilongero lililopo Wilaya ya Singida mkoani Singida akisisitiza jambo kwenye uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri mstaafu Wizara ya Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akizungumza kwenye uzinduzi huo
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Pamba cha Biosustain, Sajjad Haider  akizungumza kwenye uzinduzi huo
Wagombea nafasi ya udiwani wa jimbo hilo wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Mgombea Nafasi ya Ubunge, Haiderali Gulamali wa  Jimbo la Ilongero akiteta jambo na mke wake wakati wa uzinduzi huo.
Mke wa Mgombea Nafasi ya Ubunge, Haiderali Gulamali wa  Jimbo la Ilongero (kushoto) akiwa na mtoto wao.
Uzinduzi ukiendelea
Wananchi wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Shamrashamra zikiendelea wakati wa uzinduzi huo.
Watoto wa Gulamali wakiongoza shangwe kwenye uzinduzi huo.
Familia ya Gulamali ikifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi huo.
Familia ya Gulamali ikifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi huo.
Mgombea nafasi ya ubunge Jimbo la Ilongero akiwasili kwenye uzinduzi wa kampeni hizo.
Mgombea nafasi ya ubunge jimbo la Ilongero akilakiwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata.
Gari ya kampeni ikiongoza msafara kuelekea eneo la tukio.
Basi maalum la kampeni nchi nzima ambalo lipo chini ya Kada wa CCM Lazaro Nyalandu likiwa eneo la eneo ulipofanyika ufunguzi wa kampeni hizo.
Mgombea nafasi ya ubunge Jimbo la Ilongero akiwapungia mkono wananchi akiwa amepanda pikipiki (upande wa kushoto)
Kada wa CCM, Lazaro Nyalandu akisalimiana na wagombea nafasi za udiwani wa jimbo hilo.
Mgombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Ilongero, Haiderali Gulamali  (aliyesimama nyuma na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata, akiwa katika picha ya pamoja na wagombea nafasi ya udiwani wa jimbo hilo.
Mgombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Ilongero, Haiderali Gulamali  (aliyesimama nyuma na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata, akiwa katika picha ya pamoja na wagombea nafasi ya udiwani wa jimbo hilo.

Post a Comment

0 Comments