NYALANDU AWACHANGIA MAMILIONI WAGOMBEA UDIWANI

Subscribe Us

NYALANDU AWACHANGIA MAMILIONI WAGOMBEA UDIWANI

Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri mstaafu Wizara ya Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akizungumza katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi za CCM Jimbo la Ilongero uliofanyika Septemba 3, 2025.

............................................................

Dotto Mwaibale na Philemon Mazalla, Singida

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri mstaafu Wizara ya Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amewahangia Sh. Milioni 15 wagombea nafasi ya udiwani wa Halmshauri ya Wilaya ya Singida kupitia CCM kwa ajili ya kampeni za uchaguzi.

Nyalandu alitoa fedha hizo katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi za jimbo jipya la Ilongero lenye kata 21 uliofanyika Septemba 3, 2021.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo aliwataka kila mwananchi kila mwenye kadi ya kupigia kura kujitokeza kwenda kupiga kura nyingi kwa wagombea wanaotokana na CCM kuanzia za Rais, wabunge na madiwani.

“Tunahitaji Mkoa wa Singida uwe kinara wa kura zote katika uchaguzi mkuu na hilo linawezekana kutokana na umoja wetu tulionao”, alisema Nyalandu huku akishangiliwa.

Aidha, Nyalandu alisema atakuwa bega kwa bega na mgombea ubunge jimbo la Ilongero, Haiderali Gulamali na kuhakikisha wagombea wa CCM wanapata kura za kishindo.

“ Nitahakikisha mgombea wetu wa nafasi ya urais, wabunge na madiwani wanapata kura nyingi jambo la muhimu kila mmoja wetu siku ya upigaji kura atoke kwenda kushiriki upigaji nitaungana na timu ya taifa kwenda mikoa yote ndiyo maana kuna basi maalum kwa kazi hiyo," alisema Nyalandu.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata akiwa kwenye uzinduzi huo.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ilongero kupitia CCM Haiderali Gulamali akiwa kwenye uzinduzi huo.
Wananchi na Wana CCM wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Wagombea udiwani wateule wa Jimbo hilo kupitia CCM wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Basi maalum ambalo lipo chini ya Kada wa CCM Lazaro Nyalandu kwa ajili ya kampeni na kuomba kura za urais za Mgombea urais, wabunge na madiwani likiwa limeegeshwa wakati wa uzinduzi wa kampeni.
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri mstaafu Wizara ya Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akisalimiana na wagombea udiwani wa Jimbo la Ilongero.
 

Post a Comment

0 Comments