HARUFU YA USPIKA WA BUNGE LA TANZANIA YANUKIA KWA ZUNGU - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, November 9, 2025

HARUFU YA USPIKA WA BUNGE LA TANZANIA YANUKIA KWA ZUNGU

Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu ambaye chama chake cha CCM kimemchagua kuwa mgombea wa nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

...................................

Na Dotto Mwaibale, Dodoma

HARUFU ya nafasi ya Spika  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) inanukia kwa  Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu aliyekuwa Naibu Spika wa Bunge lililopita la 2020/ 2025 ambaye ameibuka kinara baada ya kuchaguliwa kwa kura za kutosha kuwa mgombea wa nafasi hiyo.

Zungu alipata kura 348 katika uchaguzi uliofanyika Novemba 9, 2025, jijini Dodoma   na kumshinda Stephen Masele aliyepata kura 16.

Katika uchaguzi huo Mbunge wa Babati Vijijini Daniel Sillo aliibuka mshindi kwa kupata kura 362 kwa nafasi ya Naibu Spika.

Uchaguzi rasmi wa Spika na Naibu Spika unatarajiwa kufanyika muda utakaopangwa kwa kuvishirikisha vyama vingine baada ya kupeleka majina ya washindi wa nafasi hizo wakiwemo wa CCM walioshinda na kufanya uchaguzi wa pamoja ili kumpata Spika na Naibu wake.

Wagombea wengine wa nafasi ya Uspika walijiondoa muda mfupi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo ambao ni aliyekuwa Spika wa Bunge lililopita Dkt. Tulia Ackson, Profesa Paramagamba Kabudi na Mbunge wa Isimani William Lukuvi. 

Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Daniel Sillo ambaye amechaguliwa na chama chake kuwania nafasi ya Naibu Spika.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad