HUDUMA YA NABII MKUU BALOZI DKT. GEORDAVIE M0SES YATAMBULIKA KIMATAIFA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Thursday, November 13, 2025

HUDUMA YA NABII MKUU BALOZI DKT. GEORDAVIE M0SES YATAMBULIKA KIMATAIFA


 Kiongozi wa Kanisa la Ngurumo ya Upako lenye Makao Makuu yake Kisongo mkoani Arusha Nabii Mkuu Dr. GeorDavie, akizungumza.

...............................

Na Dotto Mwaibale, simu namba (0754362990)

HUDUMA ya Nabii Mkuu, Balozi Dkt. GeorDavie Moses na Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Ngurumo ya Upako jijini Arusha imetambulika kimataifa baada ya kuteuliwa na Shirika la Mabalozi wa Amani la Umoja wa Mataifa (UN-PAF) kuwa Mwakilishi na Balozi wa Afrika Mashariki.

Kutambuliwa kwa Nabii huyo ambaye ni mlezi wa JMAT Taifa kunatokana na jitihada zake kubwa anazozifanya za ubalozi wa amani na kusaidia jamii kiuchumi na elimu ambazo zimekuwa zikionekana si kwa nchi za Afrika Mashariki bali na kimataifa.

Uteuzi huo ulifanyika Jijini New York Marekani Septemba 9, 2025 ambapo Mwenyekiti wa Dunia wa UN-PAF, Balozi Kingsley Ossai, alituma barua za utambulisho kwa Serikali ya Tanzania.

Barua hiyo pia ilitumwa United Nations Chapter ya Tanzania na Ubalozi wa Marekani nchini kwa ajili ya  kumtambulisha Dkt. GeorDavie katika wadhifa wake huo mpya.


Dkt.GeorDavie amekuwa kioo kwa jamii kwa jinsi anavyojitoa kusaidia makundi mbalimbali ya watu ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali chini ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea maendeleo na kuwainua wananchi kiuchumi. 

Baadhi ya misaada aliyoitoa hasa katika Mkoa wa Arusha ni Sh. Million 11.5 kwa ajili ya kuwsaidia watu 23 walioathirika na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa mkoani Arusha. 

Waathirika wa mafuriko hayo kila mmoja alipatiwa Sh. 500,000 ambazo zilitolewa kwa ajili ya kununua chakula, magodoro na vyombo msaada ambao ulikabidhiwa na Balozi wa Nabii huyo Mtume Sekela Ntondolo. 

Msaada mwingine ni Sh. Milioni 10 alizozitoa kwenye kituo cha kulelea watoto yatima kiitwacho Faraja Orphance Children's Home kilichopo maeneo ya Kambi ya Chupa jijini Arusha. 

Aidha Dr. GeorDavie alitoa msaada wa Sh. Milioni 100 kwa wafanyabiashara wa Soko la Samunge kwa ajili ya kukuza mitaji yao. 

Katika matukio mengine Dr. GeorDavie alitoa Sh. Milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Likamba iliyopo eneo la Kisongo barabara ambayo iliharibiwa na mvua za masika za mwaka jana. 

Mwenyekiti wa Kijiji cha Ngorbob, Mohamed Nassoro alisema Nabii huyo ametumia zaidi ya Sh. Milioni 116.5 kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo ujenzi wa maabara katika kijiji hicho. 

Msaada mwingine alioutoa ni Sh. Milioni 5 kwa ajili ya ununuzi wa vitanda 20 katika Shule ya Sekondari ya Lepurko iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Monduli. 

Hii ni baadhi tu ya misaada kati ya mingi ambayo ametoa fedha kwa ajili ya kuchangia shughuli za kijamii jambo ambalo ni zuri kwani linachagiza maendeleo ya wananchi. 

Chanzo cha Habari hii ni Arusha Digital.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad