WANAFUNZI MWAKA WA KWANZA TIA SINGIDA WAFUNDWA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Thursday, 20 November 2025

WANAFUNZI MWAKA WA KWANZA TIA SINGIDA WAFUNDWA

Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Kampasi ya Singida Dkt. David Msokwe akizungumza na Wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Taasisi hiyo wakati akifungua mafunzo ya kuwaelekeza taratibu mbalimbali za taasisi hiyo Novemba 19, 2025.

................................................

Na Dotto Mwaibale, Singida

WANAFUNZI msimu wa masomo 2025/ 2026 katika Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Kampasi ya Singida wametakiwa kufuata sheria na taratibu mbalimbali zilizowekwa na kujikita kwenye masomo na si vinginevyo.

Hayo yameelezwa na Kaimu Mkuu wa Taasisi hiyo Dkt. David Msokwe wakati akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa kwanza (Orientation for first year student) na wazamani kwa ajili ya kuwaelekeza na kuwakumbusha taratibu na kanuni za taasisi hiyo katika nyanja mbalimbali.

Alisema Serikali kupitia taasisi hiyo jukumu lake kubwa ni kuwapa elimu hivyo ni wajibu wao kuzingatia masomo wakati wote na kufuata taratibu zilizowekwa.

“Taasisi yetu ipo kwa ajili ya kuwaandaa hivyo wakati wote mkiwa chuoni hapa muwe huru kueleza changamoto zenu kwa walimu na walezi wenu ili muweze kupata msaada,” alisema Msokwe.

 Afisa Utumishi na Msimamizi wa Huduma za Rasilimali Watu na Utawala wa Taasisi hiyo, Sanura Mohamed akizungumza katika tukio hilo alisema limelenga  kuwapa uelewa kuhusu masuala ya udahili, mitihani, ulipaji wa ada, huduma za maktaba, kujisajili kupitia mfumo wa wanafunzi na kujua mazingira mbalimbali ya chuo hicho.

Alisema mambo mengine waliyoelekezwa ni pamoja na kujua huduma zingine ambazo wanaweza kuzipata nje ya masomo.

Alitaja mambo mengine kuwa ni kuvaa mavazi yenye staha kwani wanawaandaa kuwa watumishi wa baadae hivyo wanapaswa kuvaa mavazi yenye heshima, kuwa na nidhamu kwa jamii inayowazunguka na walimu.

Aidha, Sanura alitumia nafasi hiyo kuwahasa wanafunzi wa chuo hicho kutojihusisha na maandamano yanayodaiwa yatafanyika Desmba 9, 2025 yanayohamasishwa kupitia mitandao ya kijamii.

Mhandisi wa Taasisi hiyo, Godfrey Seni akizungumza na wanafunzi hao aliwata kutunza miundombinu mbalimbali ya chuo hicho kama vile samani, viyoyozi, miundombinu ya maji safi na usafi wa mazingira na kutojifanya mafundi wa kitu chochote ambacho kitakuwa kimeharibika kwani wapo mafundi kwa ajili ya kazi hiyo.

Mambo mengine waliyoelekezwa wanafunzi hao ni masuala ya Afya ya Uzazi yaliyotolewa na Mtaalamu wa Huduma Rafiki kwa Vijana katika Vituo vya Afya Manispaa ya Singida Dkt. Fatuma  Ndoile, Elimu kuhusu masuala ya mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa vyuoni iliyotolewa na Benjamin  Masyaga Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Singida.

Eneo lingine waliloelekezwa ni masuala ya Sheria yaliyotolewa na Mwanasheria wa chuo hicho Wakili Joseph Wawa, masuala ya maktaba yaliyotolewa na Mkutubi wa taasisi hiyo, Joseph Mwalubanda, masuala ya ununuzi na ugavi yaliyotolewa na Mratibu wa masuala hayo wa chuo hicho, Faraji Saidi na masuala ya Dawati la Jinsia yaliyotolewa na Innocent Msumanji kutoka taasisi hiyo.

Afisa Utumishi na Msimamizi wa Huduma za Rasilimali Watu na Utawala wa Taasisi hiyo, Sanula Mohamed, akizungumza.
Mwalimu wa Michezo wa Taasisi hiyo Mwanahamisi Mkwizu, akichangia jambo
Mtaalamu wa Huduma Rafiki kwa Vijana katika Vituo vya Afya Manispaa ya Singida Dkt. Fatuma  Ndoile akielezea kuhusu masuala ya Afya ya Uzazi kwa wanafunzi hao.
Mkutubi wa taasisi hiyo, Joseph Mwalubanda, akiwajibika
Benjamin  Masyaga Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Singida.akielezea mada yake.
Mratibu wa masuala ya Ununuzi na Ugavi wa Taasisi hiyo, Faraji Saidi akielezea mada yake.
Rais wa Serikali ya Wanafunzi (TAISO) , Maiba Tare, akizungumza.
Mhasibu wa TIA Kampasi ya Singida, Philbert Urassa, akizungumza na wanafunzi hao kuhusu ulipaji wa ada kwa wakati pamoja na mambo mengine.
Mhandisi wa Taasisi hiyo, Godfrey Seni akizungumza.
Dkt. Jonathan Majura kutoka Hospitali ya Sokoine Manispaa ya Singida akizungumza
Mwanafunzi Baraka Adamu akiuliza swali.
Mwanafunzi Sharifu Ally akizungumza.
Mwanafunzi Faith Mwita akiuliza swali.
Mwanafunzi Emmanuel Marko akichangia jambo.
Viongozi na watoa mada wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Taswira ya tukio hilo
Mwanasheria wa Taasisi hiyo Joseph Wawa akitoa mada yake
Wanafunzi wakishiriki tukio hilo.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad