Mbunge wa Jimbo la Hanang, Mhe. Asia Halamga, akiwafariji wafiwa. Mwenye koti ni Mtoto wa Marehemu Emmanuel Gamasa.
.................................
Na Dotto Mwaibale
MAJONZI, simanzi na vilio vilitawala wakati wa ibada ya
kumuaga Mzee John Gamasa kiongozi mstaafu aliyewahi kuhudumu katika nafasi
mbalimbali ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Hanang’ mkoani Manyara.
Katika mazishi yake viongozi mbalimbali wa Serikali, Chama
cha Mapinduzi, dini, madiwani pamoja na wananchi wa Jimbo la Hanang walihudhuria
yakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Hanang, Mhe. Asia Halamga.
Wakati wa uhai wake Mzee Gamasa aliwahi kuhuduma katika chama
hicho katika nafasi mbalimbali ikiwemo ya Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya
ya Hanang’.
“Mzee Gamasa tutamkumbuka kwa utendaji wake wa kazi alikuwa
ni mtu aliyeipenda kazi yake na jinsi alivyokuwa akishirikiana na wenzake
hakika ameacha alama,” alisema mmoja wa madiwani.
Mbunge wa Jimbo la Hanang, Mhe. Asia Halamga, akizungumza wakati wa mazishi yake yaliyofanyika Desemba 15, 2025 Kata ya Balang'dalalu
alianza kwa kutoa pole kwa familia ya
marehemu, ndugu, jamaa na marafiki.
” Marehemu John Gamasa alikuwa kiongozi mwenye mchango
mkubwa katika jamii na taifa kwa ujumla mambo yake yote mema aliyotuachia
tutayaendeleza na kuyaenzi,” alisema Mbunge Halamga.
“Tutaendelea kumuenzi mzee wetu John Gamasa kwa kusimamia
maadili, hekima na uzalendo alioutamani uendelee kukua katika jamii yetu,”
amesema Mhe. Asia Halamga.
Halamga alisema Mzee Gamasa alikuwa msimamizi mzuri wa
maadili, mzalendo, mwenye hekima na alikuwa ni rafiki wa kila mtu hivyo
wanapaswa kuyaishi maisha yake.
Akizungumza katika mazishi yake Mkuu wa Wilaya ya Hanang,
Mhe. Almishi Hazali, alisema amepokea kwa uchungu taarifa ya kifo cha Mzee Gamasa
na kumuelezea kuwa alikuwa mpole, mnyenyekevu, na mpenda amani mambo
yaliyofanya apendwe na kila mtu na kuheshimiwa.
Emmanuel Gamasa akizungumza kwa niaba ya familia alitoa shukrani
kwa wote walioshiriki katika msiba huo kwa namna moja au nyingine na kueleza
hiyo ni ishara ya upendo na mshikamano.
Mbunge wa Jimbo la Hanang, Mhe. Asia Halamga, akiwa na wafiwa..
Mashada yakiwekwa kaburini
Picha zikipigwa mbele ya kaburi la Mzee John Gamasa.
Mazishi ya Mzee Gamasa yakifanyika.








No comments:
Post a Comment