....................................
Na Dotto Mwaibale
MCHUNGAJI Yona Ezekiel Kanisa la Moravian Parishi ya Sabasaba
(Mandewa) Singida ahitimisha Kipindi
Cha Majilio kwa kusema yafuatayo ofisini
kwake Kwa njia ya mahojiano
MAJILIO
– MAANA YAKE NA UMUHIMU WAKE KWA WAKRISTO
MAJILIO ni Neno la kilatini likiwa na maana ya Advent Kwa
maana iyo Kwa tafsiri ya jumla ni wakati wa kuja.
JAMBO LA KUFAHAMU
Katika kitabu Cha Kiongozi Kalenda ya Kanisa Moravian
Tanzania inaonyesha kipindi Cha MAJILIO ni mwaka mpya wa kanisa yaani mwaka.
A.ndio maana tunaanza na majilio na hata masomo ya injili hasa siku za ibada ya
jumapili yamepangwa Kwa mtiririko unaofuatana
JUMAPILI YA MWISHO KABLA YA MAJILIO
Kwa mujibu wa Kitabu Cha Kiongozi Kalenda jumapili hii
inaitwa jumapili ya MFALME KRISTO
ANATAWALA. Jumapili hii tayari inaanza kuwaanda wakristo kuanza kipindi
cha majilio
YALIYOMO KATIKA KIPINDI CHA MAJILIO
Kwa watu walio wengi wanakuwa na ufahamu kuwa Christmas
imekaribia ni kweli kabisa wapo sawa lakini kanisa katika kipindi hiki cha majilio
linatafakari hasa juu ya kurudi kwa mara ya pili kwa Bwana wetu Yesu KRISTO
hapa tunakumbushwa atakaporudi Kwa mara ya pili
a) Hatakuja Kwa unyonge na udhaifu
b) Atakapokuja kwa mara ya pili atakuja kama muhukumu
c) Atakuja kama mfalme
KIPINDI HIKI WAKRISTO WANATAKIWA KUFANYA NINI?
.Kutafakari mambo yapaswayo kufanya wanaposubiri kurudi kwa
mara ya pili kwa Bwana wetu Yesu KRISTO
•Wakristo wanatakiwa kutumia muda mwingi kwa ajili ya
maombi na sala maana maombi ni sehemu ya kumsubiri Yesu Kristo anaporudi tena
•Kuendelea kukaa katika neno la Mungu
•Kujilinda na dhuluma,choyo,ugomvi na mambo yote
yatakayotufanya kukaa mbali na Mungu
MSHANGAO WA WENGI
Ni kwamba mbona habari ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo imesemwa kwa muda mrefu sana? nataka niseme mitazamo ya tofauti tofauti toka Kanisa la awali ndio maana tutaona baadhi ya nyaraka za mtume paulo hasa 2WATHESALONIKE 2:1-12 Paulo inaeleza juu ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Paulo anawahimiza Wathesalonike kusimama imara, akiwahakikishia kwamba hatimaye Yesu ataiharibu dunia hii kwa pumzi Yake, na kuwafariji walio katika taabu na kwamba hukumu ya Mungu itawashukia waovu, na si watu Wake.
Kifungu hiki ni wito wa
utambuzi dhidi ya mafundisho ya uwongo na ukumbusho wa kubaki waaminifu katikati
anaahidi kwamba Bwana Yesu atamwangamiza yule mwasi, na kuleta uharibifu wa
haraka kwa wale walioendeleza udanganyifu na kukataa upendo wa Mungu kwa ile
kweli.
LAKINI NI MUHIMU
TUFAHAMU ZAIDi
•Siku ya kurudi haijulikani
•Lini atakuja haijulikani
•Twatakiwa kubaki katika hali ya kungoja
kIPINDI
CHA KUJIANDAA
Yale yakujiandaa Bwana wetu Yesu krsto ameyafundisha kwa
uwazi tena Kwa mifano
1.MFANO
WA KWANZA
Wanawali kumi. Mathayo 25:1-13
Kama hiyo mistari ya Mathayo 25 inavyoelezea, kwamba wote walikuwa ni wanawali ikiwa na maana kuwa wote ni wakristo wanaomngojea Bwana.
Na yale mafuta waliokuwa nayo wote ni “Roho Mtakatifu”. Lakini wengine
walionekana kuwa na mafuta ya ziada, na wengine hawana.Hii inafunua aina mbili
za wakristo watakaokuwepo siku za mwisho,
AINA YA KWANZA: Hawa ni wale wakristo werevu waliopokea
Roho Mtakatifu na kuruhusu Roho wa Mungu kufanya kazi ndani yao kwa kutaka
kujifunza na kuendelea kupokea mafunuo zaidi ya Roho wa Mungu mpaka kufikia
cheo cha utimilifu Kristo (Waefeso 4:13), mtu wa dizaini hii kila siku anakuwa
tayari kujifunza jambo jipya, hivyo anahama kutoka utukufu hadi utukufu kila
siku kiu na bidii ya kuendelea kumjua Mungu
AINA YA PILI: Hawa ni wale wakristo waliojilegeza na
kujisahau ambao walishapokea Roho Mtakatifu (ambayo ndio yale mafuta kwenye taa
zao) lakini sasa baada ya kupokea Roho wa Mungu WANAMZIMISHA ndani kwa kutomruhusu
tena aendelee kuwafundisha mambo mapya, na kuwatoa hatua moja ya kiroho hadi
nyingine. Kwasababu kumbuka kazi ya Roho Mtakatifu ni kutuongoza katika kuijua
kweli yote,
2.MFANO
WA PILi
Bwana aliyesafiri na kurudi kutaka taarifa kwa watumishi
wake
Mathayo 25:14-30
3.MFANO
WA TATU
Siku atakayogawa kondoo na Mbuzi
Mathayo 25:31-46
WAPENDWA ni muhimu kufahamu kuwa maisha ya kila siku ni
majilio ya kugonja na kusubili dumuni katika wema na mema ili atakapokuja
atukute tupo tayari








No comments:
Post a Comment