Nilipoolewa, nilijua ninaingia kwenye familia yenye ukaribu. Mume wangu alikuwa karibu sana na mama yake, jambo ambalo wengi waliniambia ni la kawaida. Alisema ni mapenzi ya mama na mwanawe, na kwamba hakuna cha kushangaza.
Nilijitahidi kuelewa, nikajipa moyo, na nikamwambia nafsi yangu kwamba labda mimi ndiye nilikuwa na wivu usio na msingi.
Lakini kadri siku zilivyopita, kulikuwa na vitu vilivyonifanya nikose amani.
Uamuzi wa mume wangu ulionekana kuongozwa zaidi na mama yake kuliko familia yetu. Kila jambo ninalopendekeza lilipingwa, kila mpango ulivunjwa, na mara nyingi nilijikuta nipo pembeni kana kwamba mimi si sehemu ya maisha yake.








No comments:
Post a Comment