.............................
Na Dotto Mwaibale
Mwalimu Helena Mahamba (42) mkazi wa Unyankhae Manispaa ya
Singida ambaye kwa miaka 15 anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari anaomba msaada
wa matibabu ili aweze kupona na kuondokana na madhira anayoyapitia.
Mwalimu huyo anaishi kwa kujidunga insulin baada ya kongosho kushindwa kufanya kazi na
ametokwa vidonda katika sehemu ya mwili wake na kumfanya hashindwe kufanya kazi
yoyote zaidi ya kulala kutokana na kujisikia uchovu wakati wote.
“Ugonjwa huu umeharibu kabisa mfumo mzima wa mmeng’enyo wa
chakula na mifumo mingine ya mwili wangu nawaombeni watanzania nisaidieni
mwenzenu sina furaha kabisa ya maisha,” anasema Mahamba huku akionesha kukata
tamaa kabisa ya maisha.
Mahamba anasema alipokuwa bado msichana alianza kusumbuliwa
na presha kwa kipindi cha mwaka mmoja alipokwenda hosptali na kufanyiwa vipimo
ndipo alipogundulika kuwa na ugonjwa wa kisukari ambao umerudisha nyuma maisha
yake.
Anasema licha ya kupata matibabu katika hospitali mbalimbali
bado hajapata nafuu kila siku mwili wake umekuwa ukidhoofu huku
akiandamwa na madeni.
Anasema hata utendaji wake wa kazi umeteteleka ambapo
alilazimika kuhamia shule iliyojirani na mjini kutoka shule ya pembezoni mwa
mji alikokuwa akifundisha ili iwe rahisi kupata huduma ya hospitali ambapo
anaushukuru uongozi wa Manispaa ya Singida (mwajiri wake) kwa kumsaidia
kutokana na changamoto aliyonayo.
Anasema alipokwenda Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini
Dodoma aliambiwa matibabu yake ni Sh. Milioni 4.8 fedha ambazo ameshindwa
kuzipata.
Ndugu watanzania kila mmoja kwa imani yake, iwe taasisi
yoyote ya kiserikali, sekta binafsi, wafanyabiashara na mtu mmoja mmoja
mwenzetu Mwalimu Helena amekuja kwetu
anahitaji msaada apate fedha zitakazo msaidia kupata matibabu ya uhakika baada
ya kuangaika kwa zaidi ya miaka 15.
Mwalimu huyu ambaye ni mama wa watoto wawili tegemeo lake
kubwa kwa sasa amelielekeza kwa watanzania shime anaomba tumsaidie kwa kila
hali iwe fedha na ushauri atashukuru.
Kwa yeyote atakayeguswa kumsaidia anaweza kuwasiliana naye moja kwa moja kwa namba 0787820053/ 0759521565 au Akaunti Namba 0152364578800 Benki ya CRDB Jina Helena Nyahuru Mahamba na Mwenyezi Mungu atakubariki kwa utoaji wako kwani kiasi chochote utakacho mpa kitamsaidia ili kufikisha pesa hiyo inayohitajika kwani wahenga walisema chururu si ndo-ndo-ndo.
Mwalimu Helena Nyahuru MahambaTaarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990







No comments:
Post a Comment