Kuna deni linalokunyima usingizi. Unaamka nalo. Unalala nalo.
Kila simu ikiita moyo unashtuka ukidhani ni mkopeshaji. Hivyo ndivyo maisha
yalivyokuwa kwa Samuel, mfanyabiashara wa vipuri vya magari kutoka Industrial
Area, ambaye alijikuta akizama katika deni la zaidi ya laki saba baada ya
biashara kuyumba ghafla.
Samuel alikuwa amechukua mkopo kupanua duka lake. Mambo yalikuwa
mazuri mwanzoni. Lakini ushindani uliongezeka, wateja wakapungua, na mzigo wa
marejesho ukaanza kumlemea. Kila mwisho wa mwezi ulikuwa vita.
Simu za wadai zilianza kuwa nyingi. Baadhi walimtishia
kutaifisha mali. Alianza kukwepa simu. Alianza kukwepa hata marafiki.
Msongo Uliokaribia Kuvunja Kila Kitu








No comments:
Post a Comment